Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 152 | 2025-02-07 |
Name
Conchesta Leonce Rwamlaza
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -
Je, lini Serikali itatunga sheria itakayolinda utoaji wa huduma za matibabu bure kwa wazee na watoto?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imetunga Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023, ambayo imeanzisha mfuko wa kuhudumia makundi ya watu wasio na uwezo yakiwemo makundi ya wanawake wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
Mheshimiwa Spika, kuanza kutekelezwa kwa sheria hii kutawezesha makundi yote yakiwemo ya wazee na watoto kupata huduma za matibabu pasipo kuwepo kwa vikwazo vya fedha.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved