Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 155 | 2025-02-07 |
Name
Najma Murtaza Giga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -
Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha watoto wachanga wa wasichana wanaoendelea na masomo wananyonya maziwa ya mama kwa wakati?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kulingana na mwongozo wa wanafunzi wanaorejea shuleni baada ya kujifungua, hawaruhusiwi kwenda shuleni na watoto wao na badala yake, mwongozo unawataka wazazi kusaini makubaliano na uongozi wa shule ya kuwajibika kuwalea watoto wa wanafunzi wanaorudi shuleni. Hata hivyo, kupitia elimu nje ya mfumo rasmi, wanafunzi wenye watoto wachanga wanaruhusiwa kunyonyesha kwenye kituo.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki katika vituo vya elimu nje ya mfumo rasmi, kwa kujenga chumba maalumu cha watoto katika vituo vyote vipya vinavyojengwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari kwa njia mbadala, ambapo katika vituo hivyo, kuna mlezi anayekaa na Watoto, na mwanafunzi mwenye mtoto anapata nafasi ya kunyonyesha mtoto wake kwa wakati, pindi anapohitajika kufanya hivyo. Nakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved