Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 157 | 2025-02-07 |
Name
Kavejuru Eliadory Felix
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Buhigwe
Primary Question
MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza migogoro ya mipaka kati ya wananchi na hifadhi za misitu nchini?
Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imechukua na inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kutatua migogoro baina ya hifadhi na wananchi nchini. Hatua kubwa ambayo imechukuliwa ni uamuzi wa Mheshimiwa Rais kuunda Kamati ya Mawaziri wa Kisekta toka Wizara nane kubaini na kushauri kuhusu utatuzi wa migogoro hiyo nchini. Kamati hiyo ilibainisha migogoro 975 ambapo migogoro 438 ilibainishwa kuhusu hifadhi za misitu.
Mheshimiwa Spika, katika kutatua migogoro hiyo, tayari Wizara kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania imefanya marejeo ya migogoro hiyo, ambapo migogoro 416, sawa na 95% ya migogoro iliyokuwa imebainishwa imetatuliwa. Migogoro 22 sawa na asilimia tano ipo katika hatua mbalimbali za utatuzi, hususan ile inayohitaji wananchi kuhamishwa kupisha uhifadhi katika maeneo yaliyoonekana yabaki na hadhi ya uhifadhi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved