Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 2 | Good Governance | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 24 | 2025-01-29 |
Name
Janejelly Ntate James
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza:-
Je, Serikali imejipangaje kukwamua watumishi walioathiriwa na Mwongozo wa Upandaji Madaraja wa Miaka Minne?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikichukuwa jitihada mbalimbali za kuoanisha na kuwianisha upandishaji wa vyeo vya watumishi ambapo katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imewapandisha vyeo watumishi 180,000 wakiwemo watumishi walioathirika na zoezi hilo. Aidha, katika utekelezaji wa Ikama na Bajeti ya mwaka 2023/2024, Serikali imewapandisha vyeo watumishi zaidi ya 232,530 wakiwemo walioathirika na zoezi hilo, uhakiki wa vyeti fake na watumishi hewa. Ninashukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved