Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 2 | Finance and Planning | Wizara ya Fedha | 28 | 2025-01-29 |
Name
Janeth Maurice Massaburi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kubwa ya elimu kwa umma kwa masuala mbalimbali yanayotarajiwa kutekelezwa nchini?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa utoaji wa elimu kwa umma kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya jamii. Katika kuhakikisha kuwa jamii inapata uelewa wa kazi mbalimbali zinazotekelezwa na Serikali. Wizara zote na taasisi zake zinasisitizwa kutenga fedha kwenye mafungu yao kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma kuhusu utekelezaji na mafanikio ya shughuli na miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa muundo na mgawanyo wa majukumu ya Serikali, jukumu hili linatekelezwa na Idara ya Habari Maelezo, Wizara ya Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa pamoja na vitengo vya mawasiliano Serikalini katika Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi zote. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved