Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Janeth Maurice Massaburi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kubwa ya elimu kwa umma kwa masuala mbalimbali yanayotarajiwa kutekelezwa nchini?
Supplementary Question 1
MHE. JANETH M. MASSABURI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Je, Serikali imejipangaje kufanya kampeni kabambe ya elimu kwa umma kwa maeneo ambayo yataleta tija kwa wananchi na hata kwa Taifa? Maeneo kama kilimo cha kisasa, mtu ni afya, usalama barabarani, upandaji wa miti na utunzaji wake, elimu ya makuzi ya vijana na elimu ya mlipakodi. Ninakushukuru. (Makofi)
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massaburi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imejipanga katika mikakati mbalimbali kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vyetu vyote,vya habari TV, magazeti na mabango mbalimbali. Ninamwomba Mheshimiwa Mbunge, hata yeye asaidie katika kueleza na kutoa elimu kwa umma kwa mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana hasa Awamu hii ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved