Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 2 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 29 | 2025-01-29 |
Name
Anton Albert Mwantona
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rungwe
Primary Question
MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-
Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Barabara ya Katumba Mbambo hadi Tukuyu?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa Barabara ya Katumba – Mbambo – Tukuyu yenye urefu wa kilometa 83 kwa awamu. Sehemu ya kutoka Lupaso – Mbambo kilometa 20 na kutoka Kabanja hadi Tukuyu kilometa saba ujenzi kwa kiwango cha lami umekamilika. Sehemu iliyobaki ya kutoka Katumba – Lupaso kilometa 35.3 na Mbaka – Kibanja kilometa 20.7 mikataba ya ujenzi imesainiwa na kwa sasa mkandarasi yupo kwenye maandalizi ya kuanza kazi baada ya kulipwa malipo ya awali. Kazi zimepangwa kukamilika mwezi Mei, 2027 kwa sehemu zote mbili. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved