Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 30 2025-01-29

Name

Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE V. BUSIGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara ya Bukombe hadi Katoro kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya Bukombe – Katoro yenye urefu wa kilometa 58.20 kwa kiwango cha lami, unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Awamu ya kwanza inahusisha sehemu ya Bukombe (Ushirombo) hadi Bwenda (kilometa 5.3). Zabuni za kumpata mkandarasi zimefunguliwa tarehe 20 Januari, 2025 na kazi ya tathmini ya zabuni hizo inaendelea.

Mheshimiwa Spika, kwa sehemu ya pili ya kutoka Kashelo hadi Nyikonga (kilometa 10.4) pamoja na Daraja la Nyikonga iko katika hatua ya majadiliano. Mkataba wa kazi unatarajiwa kuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Februari, 2025. Kwa sehemu zilizobaki za Bwenda – Kashelo (kilometa 16.3) na Nyikonga – Katoro (kilometa 26.2), Serikali inaendelea kutafuta fedha, kwa ajili ya ujenzi.