Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 13 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 220 | 2025-02-13 |
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Primary Question
MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: -
Je, lini Serikali itachimba visima virefu vya maji kwenye taasisi za umma hususan mashuleni?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza inapatikana katika maeneo yote ikijumuisha taasisi za umma zikiwemo shule na vituo vya kutolea huduma za afya. Serikali huzingatia uwepo wa taasisi hizo wakati wa usanifu wa miradi ya maji na hivyo kuhakikisha zinapata huduma hiyo muhimu wakati wa utekelezaji wa miradi. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali kupitia miradi mbalimbali iliyotekelezwa imefikisha huduma ya majisafi na salama katika taasisi za umma 31,130 ambapo kati ya hizo, shule za msingi na sekondari ni 25,820 wakati vituo vya kutolea huduma za afya ni 5,310.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kufikisha huduma ya maji kwa taasisi zote za umma nchini kupitia miradi inayoendelea na inayotarajia kujengwa ikiwemo kuchimba visima virefu kadiri itakavyoonekana inafaa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved