Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 2 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 21 2025-04-09

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR aliuliza:-

Je, kwa kiasi gani Zanzibar inanufaika na fedha zitolewazo na wadau wa maendeleo kupitia Serikali ya Muungano kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada Sura 134 imeweka utaratibu wa namna Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inavyopaswa kunufaika na mikopo, dhamana na misaada kupitia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa muktadha huo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikipeleka fedha zitolewazo na wadau wa maendeleo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuzingatia Sheria hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia fedha hizo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. Miradi hiyo imewasaidia wananchi wa pande zote mbili za Muungano kushiriki na kuinua hali zao za kiuchumi pamoja na kuongeza ajira kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Ninakushukuru.