Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 39 | 2025-04-10 |
Name
Neema William Mgaya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Njombe – Kibena – Madeke - Lupembe kuelekea Mkoa wa Morogoro?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Njombe – Kibena – Madeke – Lupembe hadi Mikumi Mkoa wa Morogoro kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Sehemu ya Mikumi hadi Ifakara yenye urefu wa kilometa 109 ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami umekamilika. Sehemu za Ifakara – Mbingu kilometa 62.5 na Mbingu – Chita kilometa 37.5 kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami zinaendelea. Kwa sehemu iliyobaki ya Chita hadi Kibena, Mkoa wa Njombe kilometa 246.44, Serikali inaendelea kutafuata fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved