Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 269 | 2025-05-09 |
Name
Deodatus Philip Mwanyika
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. NEEMA W. MGAYA K.n.y. MHE. DEODATUS P. MWANYIKA Aliuliza: -
Je, lini mpango wa ujenzi wa Chuo cha Utalii katika Mji wa Njombe utaanza?
Name
Dr. Pindi Hazara Chana
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mpango wake wa kuimarisha utoaji huduma katika sekta ya utalii na ukarimu nchini, imeendelea kuimarisha Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kwa kununua nyenzo za kisasa zaidi za ufundishaji pamoja na kufungua kampasi za chuo hicho katika maeneo mbalimbali nchini ili kusogeza huduma za chuo hicho karibu na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini Serikali imeanza kuchukua hatua mbalimbali za kufungua kampasi mpya ambapo Wizara imepata eneo la takribani ekari 27 katika Kijiji cha Ikisa, Kata ya Uwemba, Halmashauri ya Mji Njombe. Aidha, hati ya umiliki wa eneo hilo tayari imepatikana na Wizara inatarajia kuanza ujenzi wa kampasi hiyo hivi karibuni kadiri fedha zitakavyopatikana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved