Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 19 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 249 2025-05-07

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:-

Je, lini ahadi ya ujenzi wa Reli ya Kusini itaanza kutekelezwa?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli (TRC) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya ujenzi wa Njia ya Reli ya Mtwara - Mbambabay na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma yenye urefu wa kilomita 1,000. Kwa sasa, Serikali inaendelea na taratibu za kutafuta mwekezaji atakayejenga reli hiyo kwa kiwango cha Standard Gauge (SGR) kwa utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP).

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumwomba Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kuwa na subira wakati Serikali ikiendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi wa reli hiyo.