Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 249 | 2025-05-07 |
Name
Agnes Elias Hokororo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:-
Je, lini ahadi ya ujenzi wa Reli ya Kusini itaanza kutekelezwa?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli (TRC) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya ujenzi wa Njia ya Reli ya Mtwara - Mbambabay na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma yenye urefu wa kilomita 1,000. Kwa sasa, Serikali inaendelea na taratibu za kutafuta mwekezaji atakayejenga reli hiyo kwa kiwango cha Standard Gauge (SGR) kwa utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP).
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumwomba Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kuwa na subira wakati Serikali ikiendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi wa reli hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved