Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 19 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 250 | 2025-05-07 |
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Primary Question
MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:-
Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Nyendara, Muhambwe, Kumbanga, Mgondogondo na Kigina, Muhambwe?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini, ikiwemo Skimu za Nyendara, Muhambwe, Kumbanga, Mgondogondo na Kigina zilizopo Jimbo la Muhambwe.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, imeanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kwa ajili ya ukarabati wa Skimu za Nyendara, Muhambwe, Kumbanga, Mgondogondo na Kigina zilizopo Jimbo la Muhambwe. Utekelezaji wa kazi za upembuzi yakinifu umefikia 70% na unatarajia kukamilika ifikapo Juni, 2025. Baada ya usanifu kukamilika skimu hizo zitatangazwa mara moja, kwa ajili ya ukarabati. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved