Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 235 | 2025-05-06 |
Name
Ally Juma Makoa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kondoa Mjini
Primary Question
MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka gari la zimamoto Wilaya ya Kondoa ili kukabiliana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha utendaji kazi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika kulipatia vitendea kazi kupitia mradi wa ununuzi wa magari na vifaa vya kuzima moto na uokoaji wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 100 kutoka Kampuni ya ADEX iliyopo Dubai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo utawezesha kupatikana kwa vitendea kazi mbalimbali ikiwemo magari 150 ya kuzima moto na uokoaji yatakayotoa huduma katika Wilaya zote nchini ikiwemo Wilaya ya Kondoa, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved