Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 236 | 2025-05-06 |
Name
Jafari Chege Wambura
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rorya
Primary Question
MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:-
Je, lini Mradi wa Maji Miji 28 Rorya - Tarime utakamilika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 wa Rorya - Tarime uliopo Mkoani Mara. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) katika Ziwa Victoria lenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 29 kwa siku, ujenzi wa miundombinu yenye uwezo wa kutibu maji lita milioni 28 kwa siku, ulazaji wa bomba umbali wa Kilometa 90, ujenzi wa matenki yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 10 sanjari na ujenzi wa kituo kimoja cha kusukuma Maji (booster station).
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 12.5%, na kwa mujibu wa mkataba unatakiwa kukamilika mwezi Julai, 2025 na kunufaisha wananchi 460,885 waishio katika Wilaya za Rorya na Tarime, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved