Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 237 2025-05-06

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali iliamua kujenga bandari Karema wakati upande wa DRC bado hawajajenga?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikishirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilisaini Hati ya Makubaliano kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha miundombinu ikiwemo bandari ili kuchochea shughuli za kiuchumi baina ya nchi hizi mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutimiza azma hiyo, Serikali kupitia TPA ilianza maboresho ya Bandari za Kigoma pamoja na ujenzi wa Bandari mpya ya Karema katika Ziwa Tanganyika. Kwa sasa TPA inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuendeleza Bandari za Moba na kwa upande wa Kalemie ujenzi umeanza kwa kushirikiana na mwekezaji. (Makofi)