Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 18 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 237 | 2025-05-06 |
Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -
Je, kwa nini Serikali iliamua kujenga bandari Karema wakati upande wa DRC bado hawajajenga?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikishirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilisaini Hati ya Makubaliano kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha miundombinu ikiwemo bandari ili kuchochea shughuli za kiuchumi baina ya nchi hizi mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutimiza azma hiyo, Serikali kupitia TPA ilianza maboresho ya Bandari za Kigoma pamoja na ujenzi wa Bandari mpya ya Karema katika Ziwa Tanganyika. Kwa sasa TPA inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuendeleza Bandari za Moba na kwa upande wa Kalemie ujenzi umeanza kwa kushirikiana na mwekezaji. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved