Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza:¬- Je, lini Serikali itajenga ukuta wa Ikulu Ndogo ya Muungano Pemba?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na shughuli iliyofanyika ya Serikali, je, Serikali ina mpango gani wa kufanya upembuzi yakinifu katika eneo lile kabla ya kujenga huo ukuta, kwa sababu hali ya pale iko mbaya kabisa, maji ya bahari yanakula katika lile eneo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri, je yuko tayari kwenda pamoja katika eneo lile kuona hasa hali halisi ilivyo katika eneo lile ambalo Serikali inataka kujenga hiyo Ikulu? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunapotaka kufanya ujenzi ama ukarabati hasa kwa jengo kubwa la muda mrefu kama lile lazima tufanye upembuzi yakinifu lakini lazima tufanye tathmini kwa ajili ya kujua gharama na mambo mengine, zaidi ukizingatia kwamba jengo lile lipo karibu ama ufukweni mwa bahari. Kwa hiyo hilo jambo la kufanya upembuzi yakinifu ni jambo la msingi na lazima tutafanya.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa kwenda, nipo tayari kwa ajili ya kwenda kukagua kuona namna ambavyo tunaweza tukaanza harakati za ujenzi katika jimbo hilo lakini pia kuona namna ambavyo limeathirika jengo hilo kwa sababu ni la muda mrefu. Baada ya Bunge hili nimuahidi Mheshimiwa Mbunge tutakuwa Wete kwa ajili ya kukagua jengo hilo.