Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari ya Hagati itapandishwa hadhi kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naishukuru sana Serikali kwa majibu haya mazuri ambayo yanaleta shangwe kubwa katika Tarafa hii ya Hagati. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shule hii ya Hagati Secondary, Halmashauri ya Mbinga ina shule ya wasichana inaitwa Mbinga Girls na yenyewe iko katika hali nzuri. Kupitia barua yenye Kumb. Na. MDC/E.80/136/135, tumeomba kibali cha shule hii nayo ichukue kidato cha tano na cha sita. Je, Serikali iko tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, halmashauri hii kwa kushirikiana na wananchi tumejenga shule za Benaya Secondary na Nguzo Secondary. Shule hizi zina upungufu wa miondombinu na sasa hivi zipo kidato cha pili. Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya miundombinu ikiwemo maabara? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Benaya Kapinga; hili la kwanza kuhusu Mbinga Girls nayo kuweza upandishwa hadhi na kuwa A – Level, Serikali ipo tayari kuweza kupandisha hadhi shule hii lakini kuna taratibu zile zilizowekwa kwa ajili ya upandishaji hadhi wa shule kuweza kuwa ya A – Level. Hivyo basi, nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbinga Vijijini kuweza kuanza taratibu za kupandisha hadhi shule hii, kwa mujibu wa sheria inavyotaka. Kwa maana lazima kwanza ifanyike assessment, pili waweze kumpeleka yule Mkaguzi wa Elimu pale na kisha waandike Wizara ya Elimu kwa ajili ya kuweza kuomba kupandisha hadhi shule hii.

Mheshmiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika shule alizozitaja ikiwemo Shule hii ya Benaya: Tutaendelea kutafuata fedha kama Serikali kwa ajili ya kuweza kuboresha miundombinu ya shule mbalimbali hapa nchini ikiwemo Mbinga DC. Hivyo basi, nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbinga DC kuweza kuorodhesha mahitaji yale ambayo yanahitajika katika shule hizi ili aweze kumwandikia Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kuweza kuona namna gani Serikali itapeleka fedha kadri ya upatikanaji wake. (Makofi)

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari ya Hagati itapandishwa hadhi kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari Kwambegu iliyoko Kata ya Mahore ambalo ni hitaji la wananchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapandisha hadhi shule hii iliyopo Kata ya Mahore. Kama nilivyokuwa nikimjibu Mheshimiwa Kapinga kwamba, ni kwa mujibu wa sheria na taratibu zile zilizopo; ni lazima kwanza iwe imekidhi vigezo ambavyo vimewekwa. Hivyo basi, nimatake Mkurugenzi wa halmashauri husika kuweza kuanza kufanya tathmini hii na kisha Mkaguzi kwenda kuona kama vile vigezo vimetimia na kuweza kuomba kwa wenzetu wa Wizara ya Elimu kuweza kupandisha hadhi shule hii. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari ya Hagati itapandishwa hadhi kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina shule moja tu ya kidato cha tano na cha sita ambayo ni Tarime Secondary, kufuatia uhitaji mkubwa wa shule za kidato cha tano na cha sita, Halmashauri ya Mji wa Tarime imeanzisha mchakato wa kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Mogabiri kwa kujenga mabweni mawili, madarasa mawili ya advance pamoja na maabara zote za sayansi.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuipandiisha hadhi shule hii ili iweze kusajili wanafunzi wa kidato cha tano Julai mwaka huu, ukizingatia tumeshakamilisha taratibu zote kama ambavyo umeainisha hapa na vigezo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwneyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko juu ya Shule hii ya Mogabiri iliyoko kule Tarime Mjini; tutakaa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Tarime Mjini kuona kama vigezo hivi vilishapitishwa na ni lini aliweza kuwaandikia wenzetu wa Wizara ya Elimu ili tuweze kufuatailia ndani ya Serikali na kuona tuweze kupandisha hadhi shule hii kama vigezo vyote vimefikiwa.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari ya Hagati itapandishwa hadhi kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 4

nakushukuru. Kutokana na umbali mrefu wa kwenda sekondari, wakulima na wafugaji wa Kata ya Nyaburundu na Kata ya Manchimweru wameamua kujenga sekondari wenyewe kwa mikono yao na sasa hivi wameshafikisha madarasa mawili.

Je, ni nini kauli ya Serikali ya kuunga mkono? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere juu ya Serikali kupeleka fedha kuunga mkono juhudi za wananchi katika Kata ya Matowelo na Nyatwindu. Nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bunda kuweza kupeleka timu kuweza kufanya tathmini juu ya mahitaji katika maeneo haya. Vilevile, nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri hii ya Bunda kuhakikisha kwamba anatenga fedha kati ya mapato yake ya ndani, kuweza kuunga mkono juhudi za wananchi hawa wa kata hizi ambazo Mheshimiwa Getere amewataja. (Makofi)