Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, lini Tume ya Umwagiliaji itatimiza ahadi yake ya kuvuna maji ya mvua katika Mbuga inayozunguka Mji wa Itigi ili kuepusha mafuriko?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali hili niliuliza Bunge la Kumi na Moja na majibu ya Mheshimiwa Omary Mgumba yalikuwa hivi hivi kwamba wataenda, akiwa Naibu Waziri wa Wizara hii. Sasa leo na mwaka huu kuna El-nino, wanatuambiaje watu wa Itigi kwamba tufe kwa sababu Serikali haitimizi ahadi? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Halmashauri ya Itigi ina scheme moja tu ya umwagiliaji na ambayo haifanyi kazi vizuri. Je, Serikali inaweza kuniahidi mbele ya Bunge lako Tukufu, kwamba wataenda kutekeleza angalau mradi mmoja wa scheme ya umwagiliaji kwa ajili ya wananchi wa Itigi wakati Wizara hiyo imepata fedha nyingi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Manyoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haina nia ya kuona wananchi wa Itigi wanakufa kwa sababu ya mafuriko. Jukumu letu sisi kama Wizara ya Kilimo ni kuhakikisha kwamba tunawajengea miundombinu itakayowasaidia wao kwenye kulima, lakini vilevile itaongeza pato ya Halmashauri ya Mji wa Itigi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilichoahidiwa katika Bunge la Kumi na Moja na ambacho hakikutekelezwa, ilikuwa ni kwa sababu ya changamoto za kifedha. Sasa hivi fedha tunayo, ndiyo maana mwaka huu tumetenga fedha na tunakwenda kulifanyia kazi. Kwa hiyo, nimwondoe shaka Mbunge kwamba, jambo hilo litafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ujenzi wa Mradi Halmashauri ya Itigi iko sehemu ya mipango yetu, kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, lini Tume ya Umwagiliaji itatimiza ahadi yake ya kuvuna maji ya mvua katika Mbuga inayozunguka Mji wa Itigi ili kuepusha mafuriko?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kulingana na mvua zinazoendelea kunyesha Wilayani Lushoto na kusababisha uharibifu hasa wa miundombinu ya barabara. Je, Tume ya Umwagiliaji haioni kwamba kuna haja ya kujenga mabwawa katika Kata za Kwai, Makanya pamoja na Ubiri? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimjibu Mheshimiwa Shekilindi kwamba mipango yetu sisi kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ni kuhakikisha tunayafikia maeneo yote yanayofaa kwa kilimo na tutahakikisha tuna-tap maeneo yote ambayo tunaweza tukapata maji ya kutosha ambayo yatasaidia kufanyika kwa kilimo katika msimu wote wa mwaka. Kwa hiyo, hata maeneo ambayo ameyataja tutayapitia tuone tutakapofanya tathmini ili kama yanafaa basi maeneo yote hayo tutayaingiza katika mpango wetu ili yaweze kutumika kwa kilimo. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, lini Tume ya Umwagiliaji itatimiza ahadi yake ya kuvuna maji ya mvua katika Mbuga inayozunguka Mji wa Itigi ili kuepusha mafuriko?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, katika Wilaya ya Shinyanga hasa vijijini kuna mbuga kubwa na mabonde. Je, ni lini Serikali itajenga mabwawa katika mbuga hizo hasa Mwakitolyo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, katika Wilaya ya Shinyanga hasa vijijini kuna mbuga kubwa na mabonde. Je, ni lini Serikali itajenga mabwawa katika mbuga hizo hasa Mwakitolyo?