Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Nsanga – Kiteputepu katika Kata ya Ntaba – Busokelo?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Mwakibete, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tunaishukuru Serikali kwa kutenga fedha hizo kwa ajili ya kujenga daraja hili, lakini kutenga ni jambo lingine, kuanza ujenzi ni jambo lingine. Je, lini ujenzi utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga kuna daraja kama hilo kutoka upande wa Isupilo kwenda Itimbo kufupisha njia ya watu wanaokwenda Iringa na kusafirisha mazao ya misitu. Je, Serikali iko tayari wakati ujao kututengea fedha ili na sisi tujenge daraja hilo?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la kwanza ni kwamba, fedha imetengwa na dhamira ya Serikali ni kutekeleza miradi kwa kadiri bajeti inavyokuwa imetengwa. Kwa hiyo kwa kadiri fedha itakapokuwa inapatikana daraja hili litajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la kuhusiana na daraja katika jimbo lake. Nimwambie pia kazi kubwa ya TARURA ni kufuatilia na kuangalia sehemu zenye mahitaji na kupanga vipaumbele. Kwa hiyo kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha na kwa kuzingatia vipaumbele daraja hilo litajengwa.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Nsanga – Kiteputepu katika Kata ya Ntaba – Busokelo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa daraja linalounganisha Kata ya Nkilizya na Kata ya Bukongo Jimboni Ukerewe limekuwa ni kilio cha muda mrefu na limekuwa linaathiri sana uchumi wa wananchi wa maeneo haya. Je, ni lini sasa daraja hili litajengwa kupitia Kijiji cha Msozi na Nkilizya?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa miundombinu hii na kwa kuzingatia vipaumbele na upatikanaji wa fedha Serikali itajenga miundombinu hii kwenye jimbo la Mheshimiwa Mbunge. Nashukuru.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Nsanga – Kiteputepu katika Kata ya Ntaba – Busokelo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri Daraja hili la Kiteputepu ni daraja ambalo linatumia mbao, linacheza na maji ni mengi sana. Wamesema kwamba wametenga na wataweka bajeti ili waweze kulifanyia kazi. Tunaomba Serikali ifanyie kazi haraka kwa maana wanawake wengi wanazama katika daraja hili pale Ntaba.

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, napokea maombi ya Mheshimiwa Mbunge, tutayachakata na nitarudisha mrejesho kwake Mheshimiwa Mbunge.