Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kumwelimisha mtoto wa kiume kujitegemea, kujiamini na kufahamu majukumu ya baba wa familia pindi anapooa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza. swali la kwanza; tumekuwa na kampeni kwa miaka mingi iliyopita, kuelimisha na kuwezesha mtoto wa kike, tukasahau mtoto wa kiume. Sasa je, Serikali ina mikakati gani kuwapa upendeleo maalum watoto wa kiume ili waweze kupata elimu nzuri na kujiamini ili baadaye waweze kuoa wanawake waliosoma?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kumekuwa na kuvunjika kwa ndoa, siku hizi ndoa zinavunjika sana na watu wanaachana sana kiasi ambacho kunakuwa na watoto ambao hawana wazazi wawili wa kuwalea. Je, Serikali ina mikakati gani katika kuelimisha, kutoa elimu kwa Watanzania hasa kuonesha majukumu ya akina mama na majukumu ya akina baba katika ndoa ili watoto hawa waweze kulelewa na wazazi wawili? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Serikali kupitia Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 inatoa haki sawa kwa watoto wote wa kike na wa kiume wakiwemo wenye ulemavu. Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa fedha nyingi kujenga madarasa katika kila mkoa kuhakikisha kwamba watoto wote wanapata elimu na waweze kufikia malengo ambayo wamekusudia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, Sera ya Taifa ya Jinsia na Maendeleo ya Wanawake ya Mwaka 2023 inatambua umuhimu wa ushiriki wa wanawake na wanaume akiwemo mtoto wa kiume kama wakala muhimu wa kuleta mabadiliko na kuimarisha maendeleo ya familia nchini. (Makofi)