Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Rwamfi?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimepokea majibu ya Serikali. Sasa kwa kuwa, kusainiwa mkataba ni jambo moja na ile miundombinu imeharibika sana na uchumi wa Nkansi sisi tunategemea kilimo na uvuvi. Tunatamini kusikia, mkataba huo utaanza lini na kukamilika ili wananchi waendelee kupata hudumu kwenye Skimu hiyo ya Rwanfi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia hekta 3,300, Wilaya ya Nkansi tuna hekta 6,145. Je, ni lini watamalizia eneo lingine lililobaki kwa sababu ndiyo uchumi wetu wa Wilaya ya Nkansi? Nakushukuru.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, namthibitishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, mara baada ya mkandarasi kusaini mkataba anatakiwa aanze kazi mara moja. Matarajio yetu ni, kwa sababu kazi ni process, ndani ya miezi 24 kazi yote iwe imekamilika na mradi uwe na full capacity.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuongeza ukubwa kutoka hekta 3,300 mpaka hekta 6,145. Hili ni lengo la Wizara kwamba, katika hatua ya kwanza tuta-deal na hizi hekta 3,300 na baada ya hapo tutaongeza miundombinu katika hizi hekta nyingine. Kwa hiyo, ni kazi ambayo ipo katika mipango yetu, ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Rwamfi?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Halmashauri ya Itigi ina skimu moja tu na haifanyi kazi vizuri. Je, Serikali sasa ipo tayari kutuongezea angalau skimu nyingine?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari kuongeza skimu katika Halmashauri ya Itigi na ipo katika mipango yetu. Ukiangalia katika mpango wa Tume ya Taifa, Itigi kuna schemes ambazo zimeongezeka pale, ahsante.