Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuongeza posho kwa Askari na Maafisa Wasimamizi wa Uchaguzi?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa katika maelezo yake amesema uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura utaenda sambamba na uboreshaji wa posho kwa mwaka 2025; ukizingatia mwaka huu tuna uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utakuwa uchaguzi wa kwanza kwa awamu ya sita: Je, hawaoni kuna haja ya kuanza kulipa posho hiyo mwaka huu ili iweze kuleta motisha katika chaguzi hizo?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Zanzibar Maafisa Usimamizi wa Uchaguzi na Askari huwa wanasimamia chaguzi mbili tofauti, chaguzi ya kumchagua Rais wa Tanzania, na wa Bunge la Muungano na chaguzi wa kumchagua Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Madiwani Zanzibar, je, hawaoni kuna umuhimu wa kulipa posho mbili? Ahsante.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni sahihi kwa mujibu wa jibu langu la msingi kama alisikiliza vizuri Waraka wa Utumishi wa Umma Na. 1 wa mwaka 2022 mwezi Mei, tayari umeshaanza kutumika. Kwa hiyo, zingatio hilo lipo pia la kuweza kulipa posho kama jinsi ambavyo ametamani kuona kwamba zinalipwa.

Mheshimiwa Spika, pili, maboresho yatafanyika wakati Tume itakapokuwa imekaa na kuanza kufanya tathmini ikiwa ni pamoja na kupitishwa kwa bajeti ya uchaguzi ya mwaka huu ambapo mazingatio hayo yote yatakuwa ndani ya bajeti.

Mheshimiwa Spika, swali la lake la pili anauliza kuhusu upande wa Zanzibar katika chaguzi kwamba ziko mbili; zile za Rais, na pia za Wabunge na Wawakilishi. Suala hili tunalichukua kama Serikali na tutazingatia kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma, ahsante.