Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa tuko katika hatua za mwisho za kupata eneo jipya katika Kitongoji cha Ipanga, naomba kupata commitment ya Serikali endapo process hizo zitakamilika. Je, Serikali itakamilisha huo mchakato haraka kwa sababu wananchi wa Mbebe wanapata changamoto sana hasa kwenye masuala ya afya?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, tunacho Kituo cha Afya katika Kata ya Isansa lakini kwa muda mrefu sana hakina wodi za kulaza wagonjwa hususan wodi ya akina mama. Naomba kujua lini Serikali itatupatia wodi za akina mama katika Kituo cha Afya cha Kata ya Isansa? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kuwapongeza wananchi wa Kata ya Mbebe kwa kuanza kutafuta eneo lingine ambalo litatosheleza ujenzi wa kituo cha afya. Nimhakikishie Mheshimiwa Juliana Shonza kwamba Serikali hii sikivu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan itatafuta fedha na kupeleka kwenye Kata ya Mbebe kwa ajili ya kuwaunga mkono wananchi kwenye ujenzi wa hicho kituo cha afya.

Mheshimiwa Spika, pili, kuhusiana na upungufu wa majengo katika Kituo cha Afya cha Isansa, naomba nimhakikishie kwamba Serikali ilishafanya tathmini kwa vituo vyote vya afya vyenye majengo pungufu ya yale yanayohitajika kwa ajili ya kutoa huduma za afya. Hivyo, tutahakikisha pia tunapeleka fedha katika Kituo cha Afya Isansa kujenga hilo jengo la wazazi na majengo mengine ili tuweze kutoa huduma nzuri zaidi kwa wananchi, ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kutosha kukamilisha Kituo cha Afya cha Ngimu katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge amefuatilia mara kadhaa na tayari tumeshakiingiza kituo hicho kwenye orodha ya vituo ambavyo vinatafutiwa fedha kwenye mwaka ujao wa fedha ili kiweze kujengewa majengo yanayopungua, ahsante.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante; wananchi wa Kitongoji cha Iringong’wen Wilayani Longido wanatembea zaidi ya kilometa 35 kutafuta huduma za afya. Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wanachi katika kumalizia zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kumkumbusha na kumsisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Longido kwa ajili ya kuanza kutenga fedha kwa awamu kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ili kuunga mkono juhudi za wananchi katika ukamilishaji wa zahanati hiyo. Pale kama mapato ya ndani hayatatosheleza, Mkurugenzi alete taarifa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili Serikali iweze kuunga mkono umaliziaji wa zahanati hiyo, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, yapo mapendekezo ya ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati katika majimbo yote Tanzania. Kwa sisi wananchi wa Kalambo, pendekezo ni katika ujenzi wa Kituo cha Afya Katete. Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na ujenzi wa vituo vya afya hivi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali kwa kuthamini afya za wananchi, ilishaweka mpango mkakati wa kutambua maeneo ya kimkakati wa ujenzi wa vituo vya afya ikiwemo vituo vya afya katika Jimbo la Kalambo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kata hiyo ambayo ameitaja alishaiwasilisha kama ni eneo la kimkakati na Serikali inatafuta fedha ili tuweze kwenda kujenga kituo hicho cha afya. Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 5

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, je, lini Serikali itaanza kuwaunga mkono wananchi wa Kata ya Msia katika ujenzi wa kituo chao cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za wananchi katika ujenzi wa vituo vya afya kwa kutoa fedha kutoka Serikali Kuu, pia kutoa fedha kutoka mapato ya ndani. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kumkumbusha na kumsisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Vwawa, Mbozi kwa ajili ya kuanza kutenga fedha za mapato ya ndani wakati Serikali Kuu ikitafuta fedha kwa ajili ya kuunga mkono, ahsante.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Mbebe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 6

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru; naomba kujua Kituo cha Afya cha Ndola ni lini kitakamilika ili wananchi waweze kupata huduma iliyokusudiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nichukue swali la Mheshimiwa Mbunge nikafuatilie kujua hicho Kituo cha Afya cha Ndola kimekwama katika hatua gani na nini kimekwamisha ili tuhakikishe tunakwamua mkwamo huo na kituo hicho tukikamilishe kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.