Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuweka utaratibu rahisi wa urasimishaji na umilikishaji ardhi hususani kwa Wanawake?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali na majibu na mradi huu wa LTIP kufanya kazi nzuri, ningependa kujua je, Serikali haioni umuhimu wa kuyafanyia kazi au kuifanyia kazi ile Ripoti ya Mapitio ya Sheria ya Kukabiliana na Migogoro ya Ardhi iliyofanyika mwaka 2020 ili sasa iweze kufanyiwa kazi, na wanawake wengi zaidi waweze kumiliki ardhi?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, napenda tu kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba haya tunayoyatekeleza sasa yameweza vilevile kuunganisha mambo mbalimbali ikiwemo hiyo taarifa iliyotolewa ya mwaka 2020 ambayo imetupa dira ya kuendelea kuhamasisha akina mama kumiliki ardhi.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kwa sasa wameongezeka kutoka 25% mpaka 41% ambalo ni ongezeko kubwa ambalo linaonesha wazi kabisa mwamko wa akina mama umeongezeka kwa asilimia kubwa sana.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuweka utaratibu rahisi wa urasimishaji na umilikishaji ardhi hususani kwa Wanawake?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na mpango huo mzuri wa urasimishaji na umiliki wa ardhi hizo, je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa nyumba zote za tope kwenye ardhi hizo? Ahsante.
SPIKA: Mheshimiwa Ntara, hebu rudia swali lako.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, pamoja na mpango wa urasimishaji na umiliki wa ardhi hizo, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba nyumba zote za tope zinaondoka kwenye ardhi hizo kabla hata hawajafanya huo urasimishaji?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ujenzi wa nyumba hizi unategemea hali halisi ya wananchi wa eneo lile. Katika namna yoyote ile, kuondoa nyumba za tope maana yake ni kuongeza uhamasishaji kwa jamii kuitumia mifumo mbalimbali ya kujipatia fedha zinazoweza zikawahamisha kutoka kwenye nyumba za tope kwenda kwenye nyumba za kisasa.

Mheshimiwa Spika, nawaomba tu Waheshimiwa Wabunge muwe sehemu ya wahamasishaji ili maeneo ambayo nyumba za tope zipo, basi tushirikiane katika kuwahamasisha wananchi wa eneo lile kutumia uchumi walionao katika maeneo hayo kuboresha makazi yao, ahsante. (Makofi)