Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Kiberashi hadi Songe Kilindi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye kipande cha makao makuu ya wilaya kwenye Kata ya Songe na Bokwa ujenzi unaendelea na sehemu zimekamilika, lakini hakuna taa na maeneo hayo yanakuwa yanapata ajali; je, Serikali ni lini itaweka taa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kipande cha Handeni – Kiberashi katika zile kilometa 20 baadhi ya wananchi wamepisha ujenzi wa kiwango cha lami lakini hawajalipwa fidia hadi leo; je, nini mpango wa Serikali wa kuwalipa fidia wananchi hawa? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kwamba makao makuu ya wilaya tunaweka taa na ndiyo kipaumbele na sasa hivi tunafanya manunuzi ya taa kwa ujumla wake. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuone kama makao makuu ya wilaya yake ipo kwenye mpango.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ulipaji wa fidia kwa wananchi hawa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba limekuwa ni suala ambalo Mheshimiwa Mbunge tunajua umekuwa unalifuatilia na sisi kama Wizara tumeshawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Fedha ili waweze kukamilisha taratibu za malipo ili wananchi hao ambao wamepisha ujenzi wa mradi huo waweze kulipwa, ahsante.