Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni kweli Mahakama hii imefanyiwa ukarabati lakini swali langu la msingi ilikuwa ni ujenzi wa majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya ya Hai. Maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Wilaya ya Hai, Mahakama zake za Mwanzo takriban zote ni chakavu, Mahakama ya Hai Kati, Masama na Boma ya Ng’ombe. Lakini Mahakama ya Mwanzo Machame tumefanya ukarabati, tena kwa kutumia vyanzo vya Mbunge mwenyewe, mimi mwenyewe na Mfuko wa Jimbo.

Swali langu, je, ni lini Mahakama hii kwa kuwa imeshakarabatiwa itafunguliwa na kuanza kufanya kazi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa Kata ya Rungugai, hususan Kijiji Kikafu Chini wanatoka mbali sana kufuata huduma za Mahakama huku Boma ya Ng’ombe.

Swali langu, je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya pale Rungugai ili iweze kuhudumia pamoja na Kata ya Mnadani?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nipende kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mafuwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake za kutusaidia kufanya ukarabati katika Mahakama ile ya Machame, na kwamba kwa sasa imeshakamilika na inangoja tu kufunguliwa. Niombe Mhimili wa Mahakama uweke ratiba ya haraka ili waweze kwenda kuifungua ile Mahakama na ianze kufanya kazi mara moja.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali dogo la pili, Kata Rungugai lini tunakwenda kujenga Mahakama pale. Ni kwamba katika utaratibu wa kawaida nadhani Waheshimiwa Wabunge wote mnao, nimewatumia kwenye mfumo, mmeona jinsi mikakati ya ujenzi tuliyonayo. Kimsingi tunakwenda kuanza ujenzi wa kila Makao Makuu ya Tarafa kupata Mahakama ya Mwanzo. Kwa hiyo kutokana na Mheshimiwa Mbunge na juhudi anazozionyesha tutampa ushirikiano wa kutosha, tutatembelea lile eneo kuona namna kama ni Makao Makuu ya Tarafa obvious ipo kwenye mpango lakini kama ni kwenye Kata tu tulishaeleza mwanzo kwamba Kata itakayopata upendeleo ni ile iliyo mbali na huduma inayotolewa kwa sasa. Kwa hiyo Mheshimiwa Mafuwe tutakuwa bega kwa bega. Kwanza kwa juhudi zako ambazo umetuonyesha hatuhitaji kukuangusha. Ahsante.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 2


MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mahakama za Mwanzo katika Jimbo la Tabora Mjini karibu zote ni chakavu ikiwemo Mahakama ya Kata ya Isevya ambayo Mahakama ile ya Mwanzo mvua ikinyesha pale Isevya hata Mahakimu wanashindwa kuingia mle ndani kwa sababu maji yanajaa kwenye ile Mahakama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati hizi Mahakama za Mwanzo katika Jimbo la Tabora Mjini?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nipende kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka Mbunge wa Tabora, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunakiri kwamba Mahakama nyingi zimechakaa sana hasa hizi za Mwanzo; na kama nilivyoeleza wakati najibu hili swali la nyongeza la Mheshimiwa Mafue; ni kwamba tunakwenda kuanza ujenzi wa Mahakama zile zilizopo kwenye maeneo ya Makao Makuu ya Tarafa. Lakini mpango wa ukarabati unaendelea wa nchi zima unaendelea katika yale majengo ambayo tunaona yanafaa kufanyiwa ukarabati. Lakini Mahakama nyingi sana za Mwanzo ni zile ambazo hazina vigezo, nyingi zilijengwa katika nyakati hizo, nyingi zinahitaji kufanyiwa maboresho makubwa na hasa ujenzi mpya kabisa.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nanafasi nami ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nitoe shukrani zangu za dhati baada ya kupata fedha kwa ajili ya jengo la Mahakama ya Wilaya, lakini ziko Tarafa za Makata, Tarafa za Kibutuka, Tarafa hizi ziko mbali sana na hazina majengo ya Mahakama.

Je, Serikali ni lini itaona umuhimu wa kujenga majengo ya Mahakama kwenye Tarafa hizi mbili?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nipende kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tunapokea shukrani zako, na huu ndio mpango kazi wa Wizara kuhakikisha tunaboresha majengo yote ya Mahakama nchini. Kuhusu Tarafa hizi mbili, tukuahidi tu kwamba katika mpango unaokuja ambao ni kuanzia bajeti hii na kuendelea tunakwenda kuanza ujenzi wa Mahakama za Makao Makuu nchi nzima. Ifikapo 2025 kila Makao Makuu ya Tarafa itakuwa na majengo mapya ya Mahakama.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Na mimi nichukue fursa hii kuishukuru Serikali kwa kutujengea Mahakama ya Wilaya ya Bunda; imekamilika na inafanya kazi. lakini katika Wilaya ya Bunda Mahakama za Mwanzo zina hali mbaya Nansimo, Jimbo la Mwibara wanatumia Ofisi ya Kata, haifanyi kazi, Mgeta, Jimbo la Bunda Vijijini, Kabasa Jimbo la Bunda Mjini, zote zina hali mbaya.

Je, ni lini mtatujengea Mahakama ya Mwanzo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nipende kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tupokee shukrani zako kwa kukiri kwamba Serikali inafanya kazi. Suala la uchakavu wa Mahakama za Mwanzo kama nilivyojibu muda mfupi uliyopita, ni kwamba tunaendelea na mkakati wa ukarabati kwenye majengo yale yanayowezekana kukarabatiwa. Lakini tunakwenda kuanza ujenzi wa Mahakama katika kila Makao Makuu ya Tarafa hapa nchini na ifikapo 2025 kama nilivyooeleza hapo nyuma nchi nzima tutakuwa na Mahakama katika kila Makao Makuu ya Tarafa. Lakini mbali zaidi ni kwamba maeneo yote ambayo tutayabaini yako mbali na Makao Makuu ya Tarafa, vilevile yanaenda kupata upendeleo.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 5

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Tarafa ya Kipatimu Jimboni Kilwa Kaskazini, shughuli za Mahakama ya Mwanzo zimekuwa zikiendeshwa katika Ofisi ya Afisa Tarafa.

Je, ni lini Serikali itawekeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo maalum kwa ajili ya shughuli za Mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Kipatimu?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis, Mbunge wa Kilwa, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza huko mwanzo, najua wazi kabisa kwamba tuna mahitaji makubwa ya majengo ya Mahakama katika maeneo mbalimbali na kwamba mpango unaokwenda kuanza sasa ni kuhakikisha kwamba tunajenga Mahakama zetu katika Makao Makuu zote za Tarafa nchini. Lakini hapa Kipatimu ambapo unapozungumzia tutaangalia kama ni Makao Makuu ya Tarafa na kwa sababu kuna ushahidi wa kutumika jengo la Katibu Tarafa, basi ni sahihi kabisa kwamba mpango huu ambao tunaanza kuutekeleza kwenye mwaka huu wa bajeti ambayo mmeipitisha tunakwenda kuanza ujenzi katika maeneo hayo ambayo yamekosa Mahakama.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 6

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Wilaya ya Mbogwe inazo Tarafa Tatu, Tarafa ya Rulembela na Masumbwe hazina Mahakama za kuridhisha.
Je, Serikali ni lini itaanza kujenga Mahakama katika hizo Tarafa ili wananchi waweze kupata huduma ya Mahakama?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maganga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli naendelea kurudia neno langu kwamba ni kweli nakiri kwamba kuna uchakavu mkubwa wa majengo katika maeneo mbalimbali ya Mahakama hapa nchini. Naomba nikiri kwamba vilevile Wizara yangu inafanya kila aina ya maboresho kwenye Mahakama na Waheshimiwa Wabunge wengi ni mashahidi tumeweza sasa hivi, tunayo miradi kama 22 kwa kipindi hiki tu cha mwaka kwa ajili ya kujenga Mahakama za Wilaya ambazo nchi nzima kila mahali pameguswa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la eneo hili la Mbogo Mheshimiwa Mbunge, nikuhakikishie Makao Makuu zote za Tarafa kwenye eneo hili zinakwenda kupata majengo mapya ambayo yatasaidia maboresho mazuri kabisa ya utoaji wa huduma za Mahakama.(Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 7

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mahakama yetu iliyopo Mlandizi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, majengo yako yako katika hali chakavu sana, hayafai hata kukarabatiwa kwa kuwa yamejengwa kwa matope, miti na kusakafiwa simenti kwa juu.

Je, ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha inatujengea majengo mapya? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mchafu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba maeneo mengi kama nilivyojieleza mwanzo majengo yake yamechakaa na mengi yalijengwa kwa kujitolea kupitia nguvu za wananchi huko nyuma na kama ilivyo Mlandizi walijenga jengo la tope.

Mheshimiwa Spika, tunakwenda kuanza ujenzi wa haraka katika maeneo yote niliyoyataja ambayo ni Makao Makuu ya Tarafa zote nchini, muda wowote kuanzia sasa baada ya bajeti hii kupita miradi mingi sana inakwenda kuanza. Kwa hiyo, naomba tu Mheshimiwa Hawa utuvumilie kidogo katika safari hii ya ujenzi wa Mahakama na muda mfupi ujao utaona mabadiliko Mlandizi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama ya Wilaya Hai kwa kuwa jengo la sasa ni chakavu?

Supplementary Question 8

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Kibiti ni moja katika Wilaya zilizopo ndani ya Mkoa wa Pwani lakini wakazi wa maeneo yale pamoja na Rufiji tunapata shida kubwa sana katika Mahakama ya Rufaa ambayo lazima waende Kibaha.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka pale Kibiti kuweza kuweza kuweka Mahakama ya Rufaa ya Kanda?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye maswali ya msingi ni kwamba tunakwenda kuanza ujenzi katika maeneo yote, ngazi ya Wilaya tunaendelea na miradi na tunayo miradi mpaka 2025 na Waheshimiwa Wabunge wote nimeshawatumia kwenye mitandao yenu, lakini kwenye Mahakama hizi za mwanzo tunakwenda kuhakikisha kwamba kwenye Makao Makuu yote ya Tarafa nchini tunapata majengo mapya ya Mahakama kwa maeneo yale ambayo hayakuwa na majengo kabisa.

Mheshimiwa Spika, vinginevyo tunaendelea na ukarabati kwenye majengo yote yanayorekebishika ambayo yanakarabatika. Kwa hiyo, tuvute subira Waheshimiwa Wabunge ni mchakato ambao kufikia 2025 maeneo yote nadhani kutakuwa hakuna maswali Bungeni kuhusu Mahakama.