Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali wa kujenga barabara na mitaro Geita Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ahadi ya Mheshimiwa Waziri ilikuwa ni kuongeza milioni 500 kuwa bilioni moja katika Barabara za TARURA, je, ni lini fedha hizo zitatoka?

Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa barabara nyingi zimekatika kutokana na athari za mvua ikiwemo Chiwale, Masasi Mkoani Mtwara. Je, Serikali ina mpango gani kupitia TARURA wa kuhakikisha barabara hizo zinapitika? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, Serikali iliahidi kweli kuongeza bajeti kutoka shilingi milioni 500 mpaka shilingi bilioni 1.5 na Serikali ina nia ya kutekeleza ahadi hiyo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kadri ya upatikanaji wa fedha, Serikali itaweza kutimiza ahadi hii na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nitalifuatilia suala hili. Tukitoka hapa tunaweza tukakutana tukazungumza ili kujua mustakabali wa masuala ya wananchi wa Geita Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, Serikali imeendelea kutenga bajeti ya kutosha na hivi sasa bajeti ya TARURA imetoka shilingi bilioni 272 na imeongezwa mpaka shilingi bilioni 710. Ni ongezeko kubwa, lakini tunatambua kwamba bado kuna mahitaji zaidi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kadri pesa zinavyopatikana Serikali inatambua umuhimu wa barabara hizi za TARURA na hasa kwa sababu zinagusa ustawi wa wananchi lakini pia zinagusa ustawi wa uchumi. Kwa hiyo, kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana Serikali ina nia ya kuhakikisha barabara hizi zinajengwa na zinafanyiwa ukarabati. Ahsante. (Makofi)