Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Boma, Kijiji cha Doma, Wilayani Mvomero?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa tuna upungufu mkubwa sana wa watumishi hasa kwenye vituo vya afya na zahanati zilizopo pembezoni, je, lini Serikali itatuongeza watumishi ili kuweza kupunguza kero hii ya watumishi iliyopo sasa hivi katika vituo vyetu na zahanati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, sera ya afya imeweka wazi kwamba kila kijiji lazima kiwe na zahanati na kila kata lazima kuwe na kituo cha afya. Mimi pamoja na wananchi wangu wa Mvomero tumeshajenga maboma zaidi ya kumi, je, lini Serikali itatupatia fedha kwa ajili ya kumalizia haya maboma ambayo tumejenga wenyewe?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali inatambua umuhimu mkubwa sana wa watumishi wa kada ya afya katika kuhakikisha huduma bora inawafikia wananchi katika vituo vya kutoa huduma ya afya msingi, tayari Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuajiri watumishi wa kada ya afya na katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali iliajiri watumishi wa kada ya afya 33, mwaka 2022/2023 Serikali iliajiri watumishi wa kada ya afya 36 na mwaka 2023/2024 Serikali imeajiri watumishi wa kada ya afya 48 katika Jimbo la Mvomero.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha inaajiri na kunakuwa na watumishi wa kada ya afya ili waweze kutoa huduma zilizo bora katika vituo vyetu vya kutolea afya msingi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili ambalo anaeleza kwamba ameweza kuwashirikisha wanchi wake katika kujenga maboma ya zahanati, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali inatambua jitihada kubwa ambayo imefanyika katika ujenzi wa maboma haya na tayari Serikali imefanya tathmini na kubaini kwamba kuna maboma ya zahanati 1,265 ambayo yatahitaji jumla ya shilingi bilioni 75.9 kuyakamilisha.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali imeweka mikakati ya kutafuta na kupata fedha kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za wananchi. Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali ipo kazini na itahakikisha inatafute fedha ili kujenga maboma hayo uliyoyataja ambayo yako katika jimbo lako.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Boma, Kijiji cha Doma, Wilayani Mvomero?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Kata ya Ilangu ni kata ya kimkakati, je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Ilangu Wilayani Tanganyika?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, kwa kutumia mwongozo na maoni ya Waheshimiwa Wabunge Serikali tayari ilishaainisha vituo vya afya vya kimkakati vya kujenga katika kila jimbo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama kituo hiki alichokitaja katika Kata ya Ilangu ni miongoni mwa vile vituo vya afya vilivyoainishwa vya kimkakati nimhakikishie Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuhakikisha inaenga vituo vya afya hivyo vya kimkakati.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Boma, Kijiji cha Doma, Wilayani Mvomero?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni lini Serikali itamalizia majengo ya zahanati katika Kijiji cha Iyayi, Uhominyi Nyawegete, Kitoho na Winome ambayo tayari yameshapauliwa na yako katika hatua za umaliziaji?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali inatambua umuhimu sana wa huduma ya afya msingi na imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha inajenga miundombinu kwa ajili ya kutoa huduma hii ya afya msingi, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali itaendelea kutafuta fedha ili iweze kukamilisha miradi ambayo tayari imeanza ikiwemo mradi alioutaja Mheshimiwa Mbunge.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Boma, Kijiji cha Doma, Wilayani Mvomero?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Kabwe kimekuwa kinatolewa kauli tofautitofauti juu ya umaliziaji wake, leo nataka kusikia kwa mara ya mwisho, ni lini mtakamilisha kituo hiki ili kianze kufanya kazi?

SPIKA: Mheshimiwa Aida Khenani kinaitwa nini ili siku nyingine ukiuliza tukukumbushe ulisema leo ni mara ya mwisho.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Kabwe, leo ni mara ya kumi nauliza.

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI tayari ilishakusanya vituo vya afya vya kimkakati vya kujengwa katika mwaka wa fedha 2024/2025 bila shaka Mheshimiwa Mbunge ulileta kituo hiki kukiombea fedha kujengwa katika mwaka wa fedha huu. Nikuhakikishie Serikali inatafuta fedha kuhakikisha kwamba vituo vya afya vya kimkakati katika majimbo yote vinajengwa na kama hiki kituo ni kituo ambacho wewe ulikileta kwamba ni kituo cha kimkakati nikuhakikishie Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Boma, Kijiji cha Doma, Wilayani Mvomero?

Supplementary Question 5

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona, Kituo cha Afya cha Mji Mdogo wa Makongolosi kimekamilika na kimeanza kutoa huduma, lakini hakina nyumba za madaktari. Chama Cha Mapinduzi Kata ya Bwawani Makongolosi wameanzisha ujenzi wa nyumba za madaktari.
Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha ili nyumba hizi za madaktari ziweze kukamilika?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kuwapongeza wananchi kwa kushirikiana pamoja kuhakikisha kwamba wanaunga mkono jitihada za maendeleo na kwa kuanza ujenzi wa miundombinu hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama vile ambavyo Serikali imekuwa ikiunga mkono jitihada mbalimbali za kuboresha miundombinu na hasa katika sekta ya afya na kuunga mkono tafsiri yake ni kupitia miradi kutoka Serikali Kuu, lakini pia kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa. Kwa hiyo, nikuhakikishie Serikali kwa utaratibu huo huo itaendelea kuhakikisha kwamba fedha zinapatikana kwa ajili ya kuunga mkono miradi ambayo inaenda kugusa miundombinu muhimu ya afya.