Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili. Swali la kwanza, Kituo hiki cha Koresa kimeahidiwa na Serikali muda mrefu. Kwa hiyo, naamini kwamba, kwa sasa katika bajeti ya mwaka huu unaokuja kitapata fedha. Je, unaweza ukatupa kauli ya kwamba kituo hiki lini kitapewa fedha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni Kituo cha Afya kule Kirua Vunjo Mashariki. Kirua Vunjo Mashariki hakuna kituo cha afya na wananchi wa pale wanafuata huduma hiyo maeneo ya mbali sana; Himo au Kirua Vunjo Magharibi na wananchi hao walikuwa hawana kiwanja, lakini wamechanga na wamenunua kiwanja cha ekari tano. Sasa tunaomba Serikali ijipange na iniambie kama wako tayari sasa kujenga kituo cha afya kwenye Kata hii ya Kirua Vunjo Mashariki? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Dkt. Kimei kwamba, Serikali inatambua, naye mwenyewe alishawasilisha maombi ya kujenga Kituo cha Afya cha Koresa na tayari tumeshakiingiza kwenye orodha ya vituo vya afya vya kimkakati. Nakuhakikishia tu kwamba, mara baada ya fedha kupatikana tutahakikisha tunazipeleka kwa ajili ya ujenzi wa kituo kile kwa sababu, ni commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba kinajengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Kituo hicho cha Afya Vunjo Mashariki kwenye kata ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja, naomba niendelee kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumeshawaelekeza Wakurugenzi wetu katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa kufanya mapping ya maeneo ya kata za kimkakati zenye idadi kubwa ya wananchi, umbali mkubwa kutoka kituo cha huduma cha jirani au eneo la kijiografia ambalo ni tata kwa ajili ya ujenzi wa vituo. Kwa hiyo, tutakwenda kufuatilia hicho kituo tuone kama kinakidhi vigezo ili kiweze kupata fedha kwa ajili ya ujenzi, ahsante. (Makofi)

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 2

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, wananchi wa Kata ya Kerenge, Kijiji cha Mayuyu, wanahemea huduma ya afya kwa umbali mrefu sana kutoka kwenye makazi yao. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza jengo la zahanati ambalo wananchi wameshajitolea na kufikia hatua ya kutandaza mkanda wa chini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Sekiboko, anafuatilia sana masuala ya afya katika Mkoa wake wa Tanga, pamoja na zahanati hiyo. Namhakikishia tu kwamba tayari tumeshaainisha hicho kituo, tunatafuta fedha kwa ajili ya kwenda kumalizia zahanati hiyo ili wananchi wapate huduma karibu zaidi, ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Bunge lililopita tuliandika maeneo ya kujenga vituo vya afya, nami kwenye Jimbo langu la Bunda nimeandika Kituo cha Afya Mihingo. Je, ni lini sasa hizo fedha za Kituo cha Afya Mihingo zitatoka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, na nitumie nafasi hii kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote. Tulipitisha hapa karatasi kwa ajili ya kuandika kata za kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika majimbo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge, orodha ile tunayo ofisini, inafanyiwa kazi, inafanyiwa makadirio ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo ambayo Waheshimiwa Wabunge mmeainisha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Getere ni suala la muda tu, tutakwenda kukamilisha utekelezaji wa ujenzi wa kituo hicho, ahsante. (Makofi)

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, ni lini Serikali itakamilisha miundombinu ya Kituo cha Afya Nakatunguru katika Wilaya ya Ukerewe ili kiweze kuwa na hadhi, kwa sababu mpaka sasa hivi hakina wodi ya wanawake, wodi ya watoto, wodi ya wazazi na miundombinu siyo rafiki sana? Nashukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna vituo vya afya ambavyo vina upungufu wa miundombinu hususani wodi za wanaume, wodi za wanawake na wodi za watoto. Tumeshaanza utaratibu wa ujenzi wa majengo ya awali kwa awamu ya kwanza na baadaye tutakwenda awamu ya pili kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo hayo ambayo yanapungua. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, kituo hicho tutakipa fedha zikipatikana kwa ajili ya kukamilisha majengo ambayo yanapungua. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana tarehe 18 Oktoba, 2023 Mheshimiwa Rais alifanya ziara Tabora. Katika ziara hiyo kwenye mkutano wa hadhara, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Mchengerwa alitangaza kwamba, tayari fedha zimepatikana kwa ajili ya kujenga vituo 214 nchi nzima. Sikonge walikuja wataalam Mwezi wa 12 wakaainisha maeneo matatu; Kiloleli, Ipole na Usunga...

MWENYEKITI: Uliza kwa kifupi.

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Je, ni lini vituo hivyo vitajengwa? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha afya ambacho ni cha kimkakati katika Jimbo la Sikonge ni miongoni mwa vituo 214 ambavyo vitaanza ujenzi wake mwaka huu wa fedha kupitia Benki ya Dunia. Kwa hiyo, nakuhakikishia kwamba, kipo kwenye orodha, na tupo katika hatua za mwisho za kuanza utekelezaji, ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 6

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza, Kata ya Ilemba na Muze ni kata za kimkakati ambazo tumeleta mapendekezo Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa ajili ya kujenga kituo cha afya. Je, ni lini mtaleta fedha hii kujenga vituo vya afya katika kata hizo? Nakushukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata hiyo ya Ilemba na kata nyingine ambazo amezitaja, nashukuru kwamba wameshaleta mapendekezo Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge na Menejimenti ya Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini. Namhakikishia kwamba, tunaendelea kutafuta fedha na pia, tunakwenda kuona gharama stahili ambazo zinatakiwa ili tuweze kuanza utekelezaji kwa awamu, ahsante. (Makofi)

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 7

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Mtunda kwenye Jimbo la Kibiti ni moja ya kata za kimkakati kujengwa kituo cha afya kufuatia athari ya mafuriko iliyokuwa imeikumba kata hii. Je, ni nini mpango wa haraka wa Serikali wa kuweza kujenga kituo cha afya katika Kata ya Mtunda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata hiyo ya Mtunda ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo la Kibiti ni kweli, ameshaleta orodha hiyo kwenye lile jedwali ambalo tumeainisha kata za kimkakati, na Serikali inaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, maeneo haya ambayo yamepata mafuriko, baada ya maji kuondoka tutakuwa na mkakati mahususi kabisa kwa ajili ya kuhakikisha tunarejesha huduma za kijamii katika hali ya kawaida, zikiwepo huduma za afya. Kwa hiyo, tutaweka kipaumbele katika eneo hilo, ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji cha Koresa, Kata ya Vunjo?

Supplementary Question 8

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Nauliza leo kwa mara ya tisa kuhusu Kituo cha Afya Kabwe. Nataka kufahamu, kwa kuwa bajeti yako tayari tumeshamaliza, ni lini mtaenda kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kabwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza kwa mara ya tisa. Inaonesha ni namna gani yuko serious na Kituo cha Afya cha Kabwe. Namhakikishia tu kwamba, Serikali iko serious zaidi kuhakikisha wananchi wa Kata ya Kabwe wanapata huduma bora za afya na tayari tumeshaanza kuweka kwenye bajeti. Kwa hiyo, ni suala la muda tu, tutakwenda kutekeleza kukamilisha kituo kile, ahsante. (Makofi)