Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 1

MHE. SALIM A. HASHAM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Ikiwa Serikali imetoa shilingi milioni 900 kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga, wakati mimi mwakilishi wa wananchi nimesema hospitali ni kongwe na haikarabatiki na wao wameamua kunipa, sijui hayo maamuzi wanakuwa wameyatoa wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Je, Waziri haoni umuhimu wa kwenda kwenda nami katika Jimbo la Ulanga kuangalia hospitali hii na kuona uhalisia wa kile ambacho mimi nakiongea?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabati na ujenzi wa Hospitali za Halmashauri unategemea hali ya hospitali ilivyo na pia ukubwa wa eneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Salim Hasham kwamba hospitali ile ni kongwe na ni ya muda mrefu, lakini tathmini ya wataalam inaonesha kwamba, kuna tija zaidi kama tutafanya ukarabati na ujenzi wa baadhi ya majengo katika eneo lile lile badala ya kwenda kuanza eneo lingine ambalo lingekuwa lina cost implications kubwa zaidi. Pia ingeongeza sana gharama za watumishi na vifaa tiba kwa sababu, tungekuwa na hospitali ya zamani pia na hospitali nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, bado hatujachelewa. Tutakaa sisi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Mbunge na wataalamu kule tushauriane, na kama kuna umuhimu wa kujenga hospitali nyingine, tutaangalia vigezo hivyo na kwenda na hatua inayofuata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwa ajili ya kupitia kuona hospitali hiyo pamoja na huduma nyingine katika jimbo lake, ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Bunda, mwaka juzi, 2022, aliagiza hospitali nyingine ya halmashauri ijengwe katika Jimbo la Mwibara. Je, hospitali hiyo itajengwa lini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ya viongozi wetu wa kitaifa na maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kipaumbele namba moja katika utekelezaji wa shughuli zetu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kajege kwamba, tayari Serikali imeshaweka mpango na itaenda kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kujenga hospitali katika eneo hilo.

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 3

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa ya Manispaa ya Mkoa wa Morogoro inazidiwa na wagonjwa. Ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Morogoro ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kumwelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwamba ifikapo Ijumaa, ndani ya wiki hii, atuletea taarifa tuone wamefikia hatua gani katika ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Morogoro, wamekwama eneo gani na gharama kiasi gani inahitajika, ili tukubaliane kwa pamoja na kuhakikisha kwamba, tunakwamua mkwamo huo na hospitali hiyo ikamilike kwa wakati, ahsante.