Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Shabani Omari Shekilindi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lushoto
Primary Question
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, lini Vitongoji vya Hendelo, Ngaloi na Muheza, Lushoto, vitapata umeme?
Supplementary Question 1
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, Vitongoji vilivyopimwa toka mwaka juzi, ambavyo ni Vitongoji vya Kwemishai, Kwemkashi, Kwebarabara, Magunga, Zeta, Kiuzai, Ula, Mpalai pamoja na Mzizima, ukizingatia vitongoji hivi vina Taasisi za Dini na Shule za Msingi. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake hiyo ya kuweka umeme katika vitongoji hivyo nilivyovitaja kwa kuwa, vina sifa zote za kupata umeme?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kila Mbunge aliahidiwa vitongoji 15; hivyo vitongoji 15 tulishawahamasisha wananchi na tukawaambia wanapata umeme. Je, ni lini utekelezaji wake utaanza? Ninakushukuru.
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ninaomba nijibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge, kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika vitongoji ambavyo amevitaja, hivyo vyote vimewekwa katika mradi wa kupeleka umeme kwa vile vitongoji 15 vya kila Mbunge. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo tumeahidi, basi ndio hivyohivyo vitongoji vitapatiwa umeme.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mkandarasi, nilitaja hapo awali, ipo mikoa mitatu ambayo wakandarasi walikuwa hawajapatikana. Mbeya, Singida pamoja na Tanga, Lushoto, kwa Mheshimiwa Mbunge, Mkandarasi ameshapatikana ataenda kutambulishwa wiki hii na atakabidhiwa site. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved