Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwanza naomba niungane na wenzangu kupongeza uongozi wa Rais wetu Magufuli kwa kazi anayoifanya, kwa wote nadhani wanaona hakuna ambaye haoni na jinsi anavyotekeleza amekuwa ni mzalendo wa nchi hii pamoja na Mawaziri wake wote kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naenda ninayo yangu matatu kwa Mheshimiwa Mpango. La kwanza kuna hili la mazao ghalani ambalo limeanzishwa kwenye kahawa, korosho na pamoja na kokoa. Kuna baadhi ya haya mambo ni mageni sana sana kama haya ya kahawa na kokoa yameanza sasa hivi, lakini yameanza kwa kishindo wananchi hawatuelewi, tunashindwa kupita vijijini, naomba mpeleke ushauri ni namna gani hizi haya mazao ghalani yatakuwa yanafanywa yanawekwa na watu wana nunua namna gani. Sababu ya kuzungumza hivo kwa sababu unakuta mkulima yeye amelima amechuma na hana hela za kuwapa wale vibarua waliokuwa wanamsadia, hata mimi mwenyewe nikiwemo, lakini tumepeleka kahawa yetu hatujue bei yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo nyuma wakati tunakua kulikuwa na mauzo ya kahawa ambayo tulikuwa tunalipwa kwanza hela, lakini ikienda kuuzwa tulikuwa tunaletewa hela iliyobaki tulikuwa inaitwa mabaki. Lakini sasa hivi hawajui itauzwa bei gani, itauzwa na nani, lakini tumekusanya tumeshaipeleka kwenye vyama vyetu vya ushirika, hilo nilikuwa najaribu tu kwamba kama Serikali iliangalie hilo ili tuepukane na hayo mabomu na maswali mengi tunayoshindwa hata kuyajibu kwa hao wakulima wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu kuna kodi ambayo kwa kweli si rafiki sana hii najaribu tu kukumbusha Bwana Mpango mwaka jana niliongelea na leo nazidi kuongelea. Kuna kodi ya mahoteli ya vyumba watu waliokuwa/wanaokusanya VAT kawaida walikuwa hawadaiwi hii kodi ya chumba ya asilimia kumi kwenda kwenye Halmashauri zetu au kwenye miji yetu. Lakini imekuja baadhi ya Halmashauri zimekuwa zikidai lakini huyo mfanyabiashara ambaye atakusanya asilimia kumi ya Serikali Kuu, asilimia kumi ya Halmashauri na vilevile kuna kodi zingine nyingi kuna city service levy zote zinakusanywa na huyo huyo, je, huyu ambaye akusanyi VAT maana yake watu wote watakimbilia kwake na hili suala naomba liangaliwe kuna baadhi ya Halmashauri zimeanza hizo fujo, kuna baadhi ya Halmashauri zinataka kukusanya na kuwapeleka watu na mbaya zaidi hawatumii kama TRA wanavyosema kwamba sisi ni asilimia 18 anakuja anakuhesabia vyumba anahesabu na vyumba 50; mara 50,000, mara mwaka mzima hajui walilala watu au hawakulala anaku-charge na kukupeleka mahakamani, kwa kweli hilo ni kubwa na ni baya zaidi kwenye masuala ya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hilo uliangalie ulisimamie kwamba je, huyu anayekusanya VAT je, naye anatakiwa alipe hiyo asilimia kumi ya city service levy naomba hilo uliangalia make pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ambalo hili ni kukumbusha ndugu yangu Mpango mmefanya kazi kubwa sana nchi hii na hela zinazolipwa na wafanyabiashara na kodi zinazolipwa zinaonekana zinatumika namna gani. Alie na macho haambiwi tazama, mimi nina macho natembea nchi naona jinsi Serikali inavyofanya kazi. Lakini siamini kwamba Bwana Mpango na timu yako yote ya ukusanyaji mapato mmewahi kujiuliza kwanini watu wakimbie na kodi, kwa mfano SADC kodi zote ni sifuri, lakini mtu anashindwa kulipa, hamjiulizi ni kwa nini. Mimi nitakupa hapa kwa nini na nakukumbusha kwasabau mwaka jana nilizungumza na mwaka huu najaribu kukumbusha mamlaka zilizopo, TRA haina tatizo unapeleka wanakulipisha kodi yako, ukitoka TRA kwa mimi nizungumze mimi kama ndio mdau wa hiyo eneo nazungumza kwa upande wangu utakuja TFDA ndio waliopewa kwenye chakula na dawa kuangalia usalama wa chakula na dawa. Na wanautaraibu ambao unaeleweka vizuri, anakwambia bidhaa yako unataka kuingiza ulete tuipime tuisajili tutakupa kwa miaka mitatu, vizuri kabisa TRA anakwambia ingiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitoka TRA unakutana na TBS anakwambia upitishi huu mzigo sasa siuji nani ni nani hizi mamlaka zingejaribu kupewa kila kitu kila mamlaka nafasi yake ili watu wasiweze kukimbia, wanakimbia kwa sababu mamlaka ni nyingi, TBS ukimalizana nao anakwambia sasa kuna vipimo sasa sisi tunaoleta vikolokolo ni hatari kweli kweli, mtu wa weights and measures naye anataka apime kila chupa ya mafuta uliyoleta kila ceiling board uliyoleta, kila kigae ulicholeta mzigo hautoki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mzigo wa kutoka siku moja uliotolewa na TRA na TFDA utakwenda miezi miwili, miezi mitatu bado uko hapo hapo. Naomba hizi mamlaka na ningependekeza hizi mamlaka kila mamlaka ifanye kazi yake, lakini katika nyongeza hatutawakuza hawa wafanyabiashara wadogo, hapo Bwana Mpango uliangalie kwa kupitia mamlaka zako uangalie hasa TBS anakwambia ukifika kwenye nchi husika unatakiwa ukapate certificate ya kila aina ya mzigo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nishazungumza tena na hili nakukumbusha tu, wewe ni mfanyabiashara mdogo umeenda ku-consolidate container una bidhaa aina kumi utafute makampuni kumi yote yakupe certificate na wewe ulikwenda kununua kwa supplier hukunua direct kutona kwa manufacturer. Kwa kweli hiyo ni kazi ni ngumu hatuta hawa Watanzania tunaotaka kuwainua kibiashara hawataweza kuinuka au kuwe na sababu moja tu kwamba hakuna kuagiza mizigo au mizigo mbadilishe utaratibu wafanye kama wanavyofanya TFDA tusajili kwa sababu hakuna kilichofichika. Kwa mfano tunazungumza habari ya SADC, ipo SADC, Uniliver ipo SADC, hivyo unapokwenda kununua au kiwanda cha ceiling board kipo SADC sisi tuchukue kiwanda cha ceiling board kinachoelewaka na address inayoeleweka tulete TBS waisajili ili kesho na kesho kutwa nisiendelee kutaka certificate ya kila wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo mimi naamini tutawafanya Watanzania hawa ambao ni wadogo wanaotaka kukua kwa sababu amini usiamini, hakuna aliyekua, wote tulizaliwa, tukawa na siku, mwezi, mwaka, miaka mpaka tukafika ikawa S.H. Amon ikawa brand badala ya kuwa jina ikawa ni brand. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo Bwana Mpango, kwa hiyo kama mimi nimefika pale nina vifurushi vyangu vya tani moja kwa nini nisiende porini pamoja na kwamba ni zero rated hata kama ni zero rated kwa nini mimi niende nikasumbuke nikae miezi kufuatilia? Nitapita porini na ndiyo maana unakuta watu wanapita porini, mngejiuliza hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka yetu iko wazi, hilo ulielewe na ndiyo maana nakuambia kwamba TRA wewe kwa mfano umenunua mzigo South Africa hujashuka hapa unakuta karatasi zako zipo tayari za kwenda kulipia ushuru na unalipa. TFDA tayari ulishafika unalipa, lakini ukianza kusema kila item uende ukalipie, ununue ceiling board waende wakakague, ununue sijui kigae waende wakakague. Naomba sana sana ili watu wasiende porini, kwa sababu hapa nchi zote za SADC hakuna kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ukiniambia VAT ni kodi mimi kwangu VAT sio kodi, mimi nakukusanyia na kukuletea, kwa sababu nitakuja kukudai, lakini unavyoniambia nikae wiki tatu na mtaji wangu ni shilingi milioni mbili haiwezekani na huwezi kuwafanya Watanzania wadogo waanze biashara na wakue. Naomba mliangelie hilo, mkae, tuweze tuwe tunapata certificate kutoka TBS kama tunavyopata kutoka TFDA na kama tunavyopata kutoka TRA hatuna matatizo nako lakini hapa pana matatizo makubwa. Mimi huo ndiyo mchango wangu na ilikuwa ni ombi langu.
(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja iendelee. Ahsante.