Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata fursa na mimi niweze kuchangia Mpango wa Serikali wa mwaka 2019. Mchango wangu umejikita kwa eneo moja kutokana na umuhimu wa eneo hilo na eneo hilo ni kilimo. Lakini kabla sijajikita kwenye mpango ningependa nitoe takwimu za umuhimu wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo kinachangia asilimia 70 ya ajira katika nchi yetu, kinachangia fedha za kigeni takribani 1.2 billion USD ambazo ni sawa na asilimia 35 ya pesa zote za kigeni zinazoingia katika nchi yetu. Lakini pia kilimo kinalisha malighafi kwenye viwanda kwa asilimia 65, kilimo kinatuwezesha kupata chakula kwa asilimia 100 katika nchi yetu, lakini pia kilimo kinachangia asilimia 29 ya pato la Taifa. Pamoja na contribution ya kilimo kwenye Taifa hili lakini Serikali ya Chama cha Mapinduzi bado haijaipa sekta ya kilimo kipaumbele, kwa nini nasema hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya mwkaa jana ilikuwa shilingi bilioni 170 pungufu ya shilingi bilioni 44 kutoka kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018. Kwa mwaka mmoja tu bajeti ya kilimo ilipunguzwa kwa asilimia 20.8 wakati wenzetu wa Kenya wanaongeza bajeti ya kilimo kutoka asilimia 2.3 kwenda asilimia tisa ya bajeti ya Taifa sisi tunapunguza bajeti ya kilimo kutoka asilimia 0.8 kwenda asilimia 5.2, are we serious kweli tunataka kutengeneza Tanzania ya viwanda? Na tunasema Tanzania ya wanyonge, Serikali ya wanyonge, hivi kuna wanyonge zaidi ya wakulima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye ukurasa wa tano wa mpango inaonyesha wka mara ya kwanza kwenye historia ya nchi yetu kilimo kilikua kwa asilimia 1.1 mwaka 2016 baada ya Serikali hii kuingia madarakani, mwaka 2015 kilikua kwa asilimia 3.4 lakini bado bajeti ilipunguzwa. Hii inaonesha Serikali hii ni adui wa wakulima kwa maana wame-focus zaidi na kipaumbele imepewa asilimia tano ya watu ambao wanaweza kupanda ndege na kutokomeza, kuwaweka asilimia 70 ya wananchi wa Tanzania wanaotegemea kilimo kwenye wimbi la umasikini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niende kwenye mpango. Niliamua nisome vitabu vitatu vya mpango ili niweze kuona trend analysis kwenye sekta tu ya kilimo, lakini pia nlitaka nijue ni kwa nini mipango ya hii Serikali haitekelezeki na badaa ya kusoma nilipata majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina kitabu hapa cha mpango 2016/2017, 2017/2018 na hiki cha taarifa ya utekelezaji wa mwaka huu na nili-focus kwenye kilimo tu kwa sababu najua tukiwekeza kwenye kilimo tunakwenda kuwatoa asilimia 70 ya Watanznaia kwenye wimbi la umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa yaani mambo niliyoyaona ni maajabu. Baada ya kusoma ni kwamba Serikali inatekeleza vitu ambavyo haikupanga, ina-report vitu ambavyo haviko kwenye mpango, inaondoa vitu ambavyo vilikuwa kwenye mpango lakini kubwa zaidi hata pesa za kutekeleza hiyo mipango pia hazipo. Ukiangalia implementation ya bajeti ya maendeleo ya mwaka jana imekuwa implemented kwa asilimia 55 tu na asilimia 45 pesa hazikwenda kwenye bajeti ya maendeleo lakini nawashangaa Waheshimiwa Wabunge, tumeacha jukumu letu tulilopewa Kikatiba la kusimamia Serikali lakini jukumu la stewardship lord tulilopewa na wananchi la kuja kuwakilisha wananchi Bungeni, tumebadilisha majukumu yetu badala ya kuisimamia Serikali tunapongeza na kushukuru, kumpongeza Rais, inasikitisha kwa kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuoneshe vituko vilivyo kwenye mpango kwenye sekta ya kilimo. Mwaka 2016/ 2017 unaambiwa ukurasa wa 70 mpaka 71 zilitengwa shilingi bilioni 4.35 fedha za ndani kuweza kuzalisha mpunga kwa tani 290,000 na sukari tani 150,000 lakini pia kupatikana kwa hati kwa mashamba makubwa kwenye Mkoa wa Katavi, Rukwa, Tabora, Lindi, Kigoma, Ruvuma, kuandaa kanzidata kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi kwenye eneo la Ludewa na Rufiji hiyo ilikuwa mwaka 2016/2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa njoo 2017/2018, hatua iliyofikiwa, kuandaliwa programu ya muda mrefu na mfupi ya upimaji wa ardhi kwa matumizi ya kilimo. Serikali imetoa shamba la ukubwa wa hekta 10,000 lililoko Mkurunge, Bagamoyo kwa Kampuni ya Bakhresa kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo cha miwa na sukari. Ukiangalia hivi vitu hata havikuzungumzwa kwenye mpango, hiyo ndiyo hatua. Kwa hiyo, mna-implement what you didn’t plan. Haya njoo sasa kwenye taarifa ya utekelezaji ni vichekesho, unaambiwa hivi; kwanza hakuna kabisa hata habari ya hilo shamba ya Bakhresa, hakuna implementation status ya hiyo tani 150,000 ya sukari pamoja na tani 290,000 na mashamba ya miwa hayajazungumziwa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja eneo la pili, tafiti za kilimo mwaka 2016/2017 milioni 854 za fedha za ndani na milioni 53 zilitengwa kwa ajili ya kuleta tani 10 za mbegu za mpunga, kukarabati na kuimarisha vituo 12 vya utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nenda sasa mwaka 2017/2018, hatua iliyofikiwa ni kuzalisha mbegu 35 mpya za mahindi haikuwepo kabisa kwenye mpango kule wanasema vitu vingine na huku wanasema vitu vingine. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vya utafiti havijazungumziwa kabisa. Kati ya tani 10 ambazo miliahidi kutekeleza ni tani 2.9. Njoo sasa kwenye taarifa ya utekelezaji ni vituko, hakuna vituo vyovyote vilivyofanyiwa utafiti, habari mpya za mbegu hazijazungumziwa kabisa. Hiyo ndiyo Serikali ya CCM ambayo inajua kupanga na kutekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nishauri kwa haraka haraka, Serikali ijenge uchumi shirikishi ambao unaweza kuhakikisha ukuaji wa kilimo unakuwa sambamba na ukuaji wa pato la Taifa. Ukiangalia kilimo kinakuwakwa asilimia 2.1 wakati pato la Taifa linakua kwa asilimia 7.1 yaani mbingu na ardhi. Ukiangalia viwanda vinakua kwa asilimia 6.8, kilimo asilimia 2.1… (Makofi)