Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia hoja iliyoko mezani na moja kwa moja ninaunga mkono maoni ya Kambi ya Upinzani ambayo yametolewa vizuri sana na Mheshimiwa Halima Mdee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana katika ule mpango ulioletwa nilizungumzia sana suala la rasilimali watu na katika ule mpango wa mwaka jana iliahidiwa kwamba shughuli zilizopangwa ni kusomesha wataalam katika fani adimu za mafuta na gesi, madaktari bingwa katika nyanja za moyo, figo, ubongo nje ya nchi na katika vyuo vya ndani vya Muhimbili na Benjamin Mkapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika taarifa ya utekelezaji hakuna mahali popote katika taarifa ya utekelezaji ambayo imetupa takwimu ya hao wataalam ambao tumewapeleka au nje ya nchi au katika vyuo tulivyovitaja na takwimu ni muhimu kwa sababu hiyo ndio itaweza kutuwezesha kupima kama tumefanikiwa au hatujafanikiwa na nikiangalia pia katika taarifa ya utekelezaji taaluma tu ambayo wapelekwa nje ya nchi ilikuwa ni wana hewa 17 ambao nafikiri ni civil avitation na injinia mmoja ndio ambayo imeoneshwa katika vitabu hiki cha utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika taarifa yako hii ya mwaka huu kuhusu suala la rasilimali watu umesema kufungamanisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu, umesema maeneo watakayopewa kipaumbele ni elimu na ujuzi hususani kusomesha kwa wingi wataalam kwenye fani na ujuzi adimu, afya na ustawi wa jamii, maji na usafi wa mazingira, vijana, ajira na wenye ulemavu, habari, utamaduni na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni suiting statement ambayo ningetegemea kwamba katika ule mpango ambao kile kitabu cha mpango mwaka huu tungenyambua to unbundle na kusema katika hizi nyanja za mkakati tutakuwa na wataalam wangapi kwa kila eneo, kwa mfano tuna mkakati huo wa ndege za Serikali, tuna hizi bombadier, tuna Dream linear ambazo zinakuja zingine, lakini sijaona popote Mheshimiwa Mpango ambapo umeainisha kwa sababu marubani wengi ni wa nje hata Mheshimiwa Ndassa pia amelizungumzia hili ni lazima tuone kinagaubaga wataalam wangapi tutawa-train. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye suala la ma- technician kwa Air Tanzania hatuna ma-technician kwa hizi ndege mpya wengi ni kutoka nje, je, Serikali ina mpango gani kuhakiksha kwamba tunakuwa na hawa ma- technician ambao watakuja kusimamia hizi ndege ili tupunguze gharama za kuwa na hawa ma-technician kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo muhimu sana tuna reli hii ya SGR tutakuwa na locomotives za za kisasa, kwenye katika taarifa iliyotolewa taarifa ni kwamba technical education tunajaribu kuongeza enrolment tunajaribu kukarabati, lakini hatujasema kwamba kweli tuna business plans ya SGR tutahitaji wataalam wangapi na tunaweka mkakati gani wa kuweza kupeleka watu hawa kuwasomesha na tupate namba, tujue ni wangapi kufuatana business plan kusudi hata hiyo reli inapokwisha tunakuwa tayari tuna wataalam kwa ajili ya hiyo reli, tuna wataalam kwa ajili ya kuendesha hizo locomotives ambazo tunategemea zitakuwa za kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mpaka sasa hivi katika suala la rasilimali watu sijaona mkakati wowote wa Serikali ambao umewekwa kushughulikia rasilimaliwatu, kwenye bajeti ya mwaka jana hakuna bajeti ambayo nimeona kinagaubaga ya kuonesha kwamba imetolewa bajeti kiasi gani kwa ajili ya mafunzo ya hawa wataalam wa mkakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukienda kwenye suala la viwanda, viwanda primary source ni kama walivyozungumza wengi ni kilimo, lakini tukiangalia bajeti ya kilimo mwaka juzi ilkuwa ni 2%, mwaka juzi ile ilikuwa 11% bado hatujaona ni jinsi gani Serikali kwa kweli iko na ari (commitment) ya kuhakikisha kwamba agriculture inahimarishwa ili iweze kutoa input kwenye viwanda ambavyo tunataka kuvitayarisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano ningetegemea kuona katika mpango numbers za Maafisa Ugani ambao watahitajika kwa ajili ya viwanda, nilitegemea kuona katika mpango tuweke ratio kwa mfano kama tunavyofanya kwa madaktari, daktari mmoja wagonjwa 8000 au 10000, tuseme ratio Afisa Ugani mmoja anategemewa ahudumie wakulima wangapi na waweze kupimwa na waweze kufuatiliwa. Kwenye hili eneo bado kazi inahitaji kufanyika kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja pia kwenye suala la sekta binafsi, inasikitisha mimi nilikuwepo kwenye reforms tulipoanzisha mambo ya PPP, lakini Serikali ya Awamu ya Tano imerudi kabisa kwenye suala la ushirikishwaji wa sekta binafsi tumeona miradi mikubwa yote badala ya kufanya sekta binafsi inafanya Serikali yenyewe, tumeona miradi kwenye Halmashauri zetu inafanya Serikali yenyewe, matokeo yake sekta binafsi imedorola, sekta binafsi ndio mwajiri mkubwa kwa hiyo watoto wetu na vijana wetu wanakosa ajira kwa sababu sekta binafsi imedorola.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kwenye uwekezaji mazingira ya uwekezaji hata kufuatana na takwimu za dunia Tanzania ni nchi ya 163 kwenye mazingira mazuri ya uwekezaji Botswana wametushinda 86, Kenya 61. Ukija kwenye urahisi wa kufanya biashara Tanzania tuko 137, Kenya wako 80, Rwanda wako 41, tukija kwenye ada za usajili za wawekezaji kuanzisha biashara Tanzania ni dola za Marekani 250, Kenya 40, Rwanda ni 35; kwa takwimu hizi sekta binafsi haitaweza kufanikiwa kwa sababu watu watashindwa kuja kuwekeza na watakwenda kwenye nchi nyingine. Kwa hiyo, nashauri Mheshimiwa Mpango na wataalam wake waendelee kuona ni jinsi gani mazingira ya uwekezaji yataborehswa ili ku-attract wawekezaji wa ndani na nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nizungumzie sasa kidogo mimi kama Waziri kivuli wa utawala bora. Utawala bora ni kichocheo kikubwa sana cha kuleta wawekezaji na unapokuwa na viongozi ambao wanatoa kauli ambazo zinakimbiza wawekezaji, viongozi wanaotoa kauli ambazo zinakinzana hata na sera na matamko ya Serikali na bila kuchukuliwa hatua zozote hii yenyewe inatosha kuwakimbiza wawekezaji wasiweze kuja kuwekeza ndani ya nchi. Kiongozi yeyote hana maoni binafsi, kiongozi anapozungumza anazungumza kwa niaba ya Serikali ni lazima matamko yake yasikinzane na matamshi ya Serikali, matamko ya Serikali na sera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.