Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi na kwanza naomba niunge hoja mkono mapendekezo ya mpango ulioletwa kwetu pamoja na mapendekezo na ushauri wa Kamati ya Bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili mpango tufanikiwe kiuchumi, tunahitaji mali ghafi inayozalishwa nchini. Kwenye kilimo ni vizuri tukatoa kipaumbele kwenye kilimo cha umwagiliaji, tunayo mabonde mengi wengine wapo kandokando na maziwa ni muhimu tukawekeza kipaumbele ili watu walime wakati wote, tunayo mifano ya wale ambao wanatumia irrigation scheme kwa mfano kule Magu tunaye Ngongoseke analima green house, ni green house nzuri ambayo imeajiri watu wengi, lakini ana uhakika na soko la biashara ya kwake. Lakini tunaye mwingine anitwa Vick Fish amewekeza vizuri, tunaye Mtemi Chenge hapa amewekeza vizuri kilimo cha umwagiliaji cha mpunga cha mfano. Kwa hiyo niombe sana Serikali tutoe kipaumbele kwenye uwekezaji wa kilimo cha umwagiliaji ili tuweze kuzalisha malighafi ambayo kimsingi itatumika viwandani ili kuhakikisha viwanda tulivyonavyo material yake yapo hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuhitaji viwanda lakini wawekezaji wetu bado wanakumbwa na changamoto nyingi kwamfano exemption ya viwanda kwa maana ya mitambo pamoja na godowns wanapata shida sana hebu tuangalie tuweze kutoa exemption ili wananchi wetu waweze kujenga viwanda baadae kodi tu watalipa. Kwa mfano wawekezaji wa wazawa ndani hatuwapi tax holiday, tukiwapa tax holiday wanapata namna ya kujenga uwezo ili baadae waweze kuimarika na kuweza kutoa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri sana Serikali yetu ambayo inahitaji kwa kweli uchumi wa viwanda, lakini ili tufikie kwenye uchumi mzuri na kuboresha mpango huu suala la Stiegler’s Gorge ni jambo muhimu sana kupewa fedha za kutosha ili tuweze kupata umeme tuweze kuendesha hii hivi viwanda pamoja na mambo mengine ambayo wananchi wanahitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu ya barabara kwa sababu tunapozungumza uwekezaji wa viwanda lazima tusafirishe malighafi, lazima tusafirishe bidhaa, ni vizuri ikawekwa kipaumbele kama ambavyo kwenye hotuba yako umesema umeliwekea kipaumbele, cha muhimu ni fedha zipatikane ili utekelezaji uwepo haraka zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo miradi ambayo wananchi wameianzisha, miradi ya afya, miradi ya elimu.

Kuna maboma mengi Ilani ya Chama cha Mapinduzi inasema zahanati kila kijiji sisi tumejitahidi kuhamasisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali wamejenga maboma ya kutosha. Kwenye mpango huu tuone namna ya kuweza kukamilisha tunapokuja kwenye bajeti tuweke fedha za kukamisha maboma haya ili wananchi waweze kupata huduma wanayoihitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe wataalam, wachumi wabobezi watueleza sisi Wabunge na watueleze wananchi hivi umaskini mnaupima kwa namna gani? Kwa sababu hapa asubuhi kila mmoja anazungumza uchumi, wabobevu wa uchumi mtueleze uchumi mnaupima kwa namna gani, kwa sababu unaweza leo wewe watu wasema wananchi hawana fedha mfukoni, unaweza ukawana na fedha mfukoni lakini huwezi kusafiri kwa sababu miundombinu haipo, huo ni uchumi; unaweza ukawa na fedha mfukoni lakini huduma ya afya ukakosa huo ni uchumi? Unaweza ukawa na fedha mfukoni ukakosa elimu nzuri huo ni uchumi? Leo vyuo vipo umaskini wa elimu watu hawana, mtueleze kwamba uchumi manaupima kwa namna gani kwa sababu nchi hii imepiga hatua sasa kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona wananchi wake leo kule vijiji wanashindana kujenga nyumba nzuri huo sio uchumi? Wanashinda kusomesha huo sio uchumi? Wanashindana kuishi maisha bora huo sio uchumi? Tunaupima uchumi kwa namna gani, uchumi wa kukosa hela mfukoni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba wachumi wabobevu mueleze jambo hili mnaupimaje, kwa sababu tumeweza kuwa tunapata taabu, halafu mimi nashangaa sana ndio maana Mwenyenzi Mungu wakati anataka kuumba nchi, mbingu na dunia hakuumba kwanza mwanadamu, aliona akiumba mwanadamu atampa taabu kuumba mambo yote ambayo aliyafikiria kuyaumba. (Makofi)

Sasa mimi niwaombe na wale wote manao hangaikia Katiba, Katiba yetu haiwezi kuwa inajadiliwa na watu 600 na kama mtaamua Serikali kuleta Katiba wakae watu wachache wabobevu, wachache waweke mpango mzuri wa namna Katiba yetu sio watu 600 ndio maana nasema hivi Mungu alipotuumba wanadamu hapa Tanzania kwa awamu hii ni kama aliumba mapacha wanne. Akamuumba John Magufuli, akamuumba Samia, akamuumba Majaliwa, akamuumba na Dkt. Mpango. Yale mnayoyafanya ninyi watu wanne fanyeni hivyo hivyo, kwa sababu tukitaka watu wote tutoe mawazo yetu tutapotosha Taifa. Kwa hiyo niwaombe sana, tunapoleta mapendekezo ya mpango kazi yetu sisi Wabunge ni kushauri ili tuweze kuboresha mpango wenyewe. (Makofi)

Kwa hiyo, Serikali imefanya kazi kubwa na naendelea kuipongeza Serikali. Leo ukienda Dar es Salaam barabara zinajengwa kila mahali, ukienda Arusha barabara zinajengwa kila mahali, ukienda Mwanza barabara zinajengwa kila mahali, ukienda Mbeya barabara zinajengwa kila mahali, tunataka uchumi wa namna gani? Tunataka viongozi wa namna gani fanyeni kazi wala msikatishwe tamaa wananchi wapo bega kwa bega na ninyi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji nchi iliyotulia, tunahitaji vyombo vya ulinzi na usalama vilinde raia wake, unajua watu tunasema watu wanakufa, duniani kote watu wanakufa na hili jambo la kawaida, unajua tusifanye iwe hoja, kutekwa kwa ma-billionaires tusifanye iwe hoja, duniani kote watu watekwa. Ndio maana vyombo vyetu vya ulinzi wa Kangi Lugola linda raia wako. Hakuna mahali popote nchi hailindi raia wake, ndio maana hata Mwenyezi Mungu kule mbinguni analindwa na jeshi kubwa la malaika, kwa hiyo, lazima watu wote walindwe, tuimalishe lakini tuwape angalau namna ya majeshi yetu kadri ambavyo wanaulinda tuwaongezee uwezo wa kuweza kukabiliana na matatizo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.