Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa dakika tano ulizonipa. Nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya na maendeleo ya nchi yetu yanavyokwenda chini ya Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka nimshauri, ni miaka mingi tu namshauri Mheshimiwa Waziri kuhusu biashara ya bandari na maeneo mengine ambayo si friendly kwa importers na exporters. Ukichukua mfano wa container la futi 20 ambalo sasa hivi gharama yake kwa Bandari ya Mombasa ni dola 80, wamepunguza kutoka dola 103. Kwa Tanzania container la futi 20 handling charges zake ni dola 170. Sasa hii haiwezi ku-attract importes kutumia Bandari ya Dar es Salaam na kuweza ku-encourage volume ya importation. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Dar es Salaam transit goods ambazo ndizo tunazozitegemea, ndiyo uzima kabisa wa bandari yetu, importation container futi 20 ni dola 100 handling charges lakini ukienda Kenya ni dola 60. Kwa hiyo, watu wengi lazima watahamia katika bandari ambayo ina unafuu. Kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Waziri aendelee kuchukua ushauri wa kutazama ni namna gani tariffs za kodi za importation za bandari zetu zitashuka, ziwe friendly kwa wafanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingine naotaka nimpe Mheshimiwa Waziri ni kutazama gharama za kodi Tanzania. Tulijaribu kumshauri Waziri siku za nyuma ajaribu kutazama na huu ulikuwa ni mpango wa siku nyingi, VAT ilipoanza ilikuwa ni 20%, ikashuka to 18% ilikuwa ni utaratibu wa Serikali kuendelea kuishusha VAT kuja 16% au hata 17% ili ku-encourage industries. Industries zikiwa encouraged ajira na growth zitaongezeka. Kwa hiyo, namuomba Waziri atazame sasa hivi suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, excise duty; soft drinks sasa hivi Tanzania production imeshuka sana kwa sababu gharama ni kubwa na wananchi hawawezi kumudu kununua maji au soda. Excise duty ukiipunguza volume ya mauzo itakuwa na production itakuwa kubwa kwa maana Serikali haitapoteza kitu, itapata mapato yake kwenye consumption tax. Mnywaji akinywa soda au maji kodi inalipwa. Kwa hiyo, naomba Waziri alitazame suala hili ili kuona namna ya ku-encourage growth. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine atazame gharama za importation ya industrial sugar. Wafanyabiashara wengi wanalalamika, wanalipa deposit ya pesa, lakini sasa ni zaidi ya miaka mitatu, minne hawarudishiwi pesa zao na imekwenda juu sasa imefika zaidi ya shilingi bilioni 45 na hii ni mitaji ya wafanyabiashara. Wafanyabiashara wanalipa kodi vizuri, Serikali ikitazama maeneo mazuri ya kukaa na kushirikiana nao mapato mengi ya kodi Serikali itayapata bila kuwa na viwango vikubwa ambavyo vinawakimbiza. Wafanyabiashara wengi sasa hivi wanaondoka kwenda nchi zingine. Ni lazima tu-attract investors kwa kuwa na tariffs nzuri na friendly za kodi nchini mwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naunga mkono hoja.