Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda kuanza kwa mambo mawili. Kuna mtu anaitwa Beno Kakolanya na kuna mtu anaitwa Cletus Chota Chama au sisi watu wa Simba tunamwita triple C, kwamba mtu anapofanya jambo jema anastahili kupongezwa, wala si dhambi kupongeza. Ndiyo maana mashabiki na wapenzi wa Yanga na hata wa Simba siku ya Simba na Yanga tulimpongeza Beno Kakolanya kwa sababu aliokoa magoli mengi ya wazi. Ndiyo maana hata wapenzi wa mashabiki wa Yanga wanampenda na kumpongeza Cletus Chota Chama kwa kwa sababu anafanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? Kuna mambo yamefanyika ni wajibu wetu kama Wabunge kupongeza na kuitia moyo Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sitaenda kwenye mengi nitaenda kwenye afya tu ukurasa wa 30, ukarabati wa hospitali za wilaya 10, vituo vya afya 295 na nyumba za watumishi 306. Kama hiyo haitoshi nikienda ukurasa wa 33 kwenye suala la elimu tumeona ongezeko la watoto kutoka milioni 1.5 mpaka milioni 2 kutokana na elimu bila malipo. Hawa watoto laki tano maana yake ni kwamba wangekosa masomo, wangekosa elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika hatua hizi tunazopiga kuna tabia inataka izuke katika taifa letu la kuzua taharuki, ni lazima tuikemee. Kuna watu wapo tayari wao kuzua sura ya hofu. Nitatoa mfano, watu wanatoa hoja hapa, hivi mimi kwa mfano kwetu Mafinga familia yangu imemuita mke wangu Mafinga, hivi wewe nyumba ya tatu


unaanza kuperuzi kwa nini ameitwa kwenda mafinga kujadili mambo yao ya familia? Watu wamemuita Balozi wao wanaenda ku-discuss issue zao why do you speculate wanaenda kujadili nini, uitake Serikali ikuambie eti ameitwa kwa nini? Thus is none of your business. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge hii hali ya kupenda kuzua hofu, jambo dogo tu kulikuza na kuleta hofu hofu; na ndiyo maana na mpongeza sana Katibu Mkuu Dkt. Bashiru katika mdahalo mmoja alipoeleza kuhusu hofu, alisema wenye hofu ni mafisadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unafanya kazi zako, unawakikilisha wananchi wako kama Chumi hapa, kwa nini usiringe?


Kwa hiyo, lazima sisi kama viongozi tuwe mstari wa mbele kueleza yaliyo mema na kuonesha mstakabali kwa lugha njema na zaidi ya yote sisi kama Bunge kushauri Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu hapa wamesema hapa FDI (Foreign Direct Investment) zimeshuka.


Nataka niwaambie globally zimeshuka kwa asilimia 23 siyo sisi tu, kutoka trilioni za Kimarekani 1.37 mpaka trilioni 1.43.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Afrika zimeshuka kwa asilimia 21, katika East Africa zimeshuka kwa asilimia 25.3 kutoka dola za Kimarekani bilioni 8.8 mpaka bilioni 6.6 na hapa anguko hilo katika East Africa sisi tuna nafuu. Ukienda Kenya ndiyo ime-record the highest anguko ni asilimia 60.6 yaani kutoka bilioni 1.8 mpaka dola milioni 717.7, Uganda anguko ni asilimia 14.2 sisi Tanzania asilimia 7 yaani ni Rwanda na Burundi tu ndiyo ambao wamekuwa na afadhali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Rwanda kutoka dola za Kimarekani milioni 600 mpaka dola milioni 1.2, hata Burundi kutoka dola za Kimarekani milioni 65 mpaka dola milioni 146. Kama una akili timamu unaweza kulinganisha dola milioni 186 ambazo zimeingia Burundi na sisi ambao tumeingiza hapa nchini dola bilioni 3.3 kama FDI? Kuna nchi zimepongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi si takwimu za Cosato Chumi, nenda kwenye ripoti ya UNCTAD (United National Conference on Trade and Development), The World Investment Report ya 2018. Katika FDI zilizokuja hapa East Africa sisi ndiyo the highest. Katika dola bilioni 4 zilizokuja katika East Africa sisi tumepata share ya 1.2 bilioni FDI, Uganda 0.7 bilioni dola za Kimarekani na Kenya 0.67 bilioni. Kwa hiyo, hata katika East Afrika yaani sisi tume-attract the highest. Sasa haya mambo pamoja na mapungufu yake lazima tupongeze halafu tuangalie sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwenye Easy of Doing Business bado hatupo vizuri, maana yake tukiwa vizuri tutavutia zaidi ya hii tumevutia. Kwanza kabla sijaenda kwenye hiyo, hizo FDI maana nisiseme tu FDI zimeleta nini? Katika East Africa sisi zimezalisha ajira zaidi ya 20,000 sawa na asilimia 20 waliotuzidi ni Uganda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nachotaka kushauri, tumesema Bunge kazi yetu ni kushauri, katika ile Easy of Doing


Business Index sisi tume-fall, tupo namba 147 ukilinganisha na Rwanda ambao ni 29 na ni kwa nini tumeanguka? Kuna mambo mengi, Mheshimiwa Dkt. Mpango pamoja na jitihada hizi za kujenga mazingira wezeshi, miundombinu, nishati na kadhalika tunalo jambo moja kama Serikali kuchelewa kufanya maamuzi. Kwa hiyo, ni lazima tuambizane ukweli Serikali kuchelewa kufanya maamuzi na kwa wakati ni tatizo. Mtu amepata work permit Labour akienda Immigration anachelewa kupata residence permit. Kuna contradiction ya maamuzi katika maeneo mbalimbali ya mamlaka, tukiweza hili maana yake ni kwamba tutavutia uwekezaji. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuboresha mazingira tuangalie pia na ndani. Haiwezekani umetoa mbao Mafinga unapeleka Mwanza unaambiwa usafiri mchana tu ikifika saa
12.00 umesimamishwa, uta-run vipi uchumi? Gari kwenda Mwanza inatumia siku nne ingetumia siku mbili au siku moja maana yake kwanza hiyo gari ingejaza mafuta mengi na Serikali ingepata fuel levy. Kwa hiyo, haya ndiyo mambo ya kuboresha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa kumalizia, lazima nimpongeze Mheshimiwa Kangi Lugola. Hata ukienda nchi za watu kuna maeneo wanafanya biashara saa 24. Huwezi ukazuia biashara za watu saa tano, hivi wewe uende pale Mikumi uwaambie wale akina mama ikifika saa tano wafunge biashara wakati wao biashara yao wanategemea watu ambao wako on transit. Uje Mafiga uwaambie kina mama ntilie wafunge biashara saa nne wakati wao client wao wanategemea vijana waliotoka msituni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna maeneo tujaribu kuboresha na wala si sheria, ni kanuni ambazo Mawaziri wanaweza wakazirekebisha ile Easy of Doing Business ikawa nzuri tukavutia foreign investment, tukapata mapato mengi ili huu mpango tukaugharamie ipasavyo kwa sababu tumeona mikopo kutoka nje na misaada haiji kwa ile pace tuliyotarajia. Kwa hiyo, kikubwa lazima kitoke ndani, kitatoka ndani vipi ni kwa kuboresha mazingira ya kufanya biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mungu awabariki kwa kunisikiliza, ahsante sana, naunga mkono hoja.