Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia fursa hii kuwa mchangiaji wa mwanzo kwa siku ya leo katika kuboresha Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwa hai na wazima hadi leo na afya njema tukaweza kuendelea na majukumu yetu, kwa hiyo naomba nianze moja kwa moja kuboresha mpango wetu huu ambao umeletwa mbele yetu katika eneo la uwezeshaji wanawake lkiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili ni muhimu sana na ndiyo maana nimelitenga kwa upekee wake niweze kulichangia kwa siku ya leo. Pamoja na kuipongeza sana Serikali kwa mkakati ambao unafanywa katika kuongeza juhudi za kuwawezesha Wanawake kiuchumi katika maeneo mbalimbali hasa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu mimi naomba nielekee kwenye maeneo hayo ambayo yanashughulikiwa hasa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la mpango wa TASAF, najua nia ya Serikali ni njema hapa lakini niseme tu kwamba mpango huu unawanufaisha wale wanawake ambao wako mfuko tu na pia hao wanawake ambao wako kwenye mfuko huu wa TASAF au mpango huu wa TASAF wananufaika kwa kiasi gani hilo hatujui, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri labda pengine ukija utueleze namna gani wanawake ambao wako kwenye mpango huu wa TASAF wananufaika kwa kiasi gani, lakini ambao awamo kwenye mpango huu hawana manufaa yoyote wanayoyapata kwa hiyo bado mpango huu haujawafikia wanawake kwa namna ambavyo inastahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuna Benki ya Wanawake ambayo imeunganishwa sasa na TPB na kufunguliwa dirisha maalum kwa ajili ya wanawake, mimi nashauri sana Mheshimiwa Waziri dirisha hili likusudiwe kwa lengo lililokusudiwa yaani lifanyiwe kwa kazi kwa lengo lililokusudiwa ikiwa ni dirisha la wanawake liwe ni la wanawake tu na kisingiie kitu kingine chochote na isiwe kwavikundi ianzie from individuals to the group ili mwanamke wa kitanzania afaidike na hii benki ambayo imewekwa kupitia TPB au dirisha hili la wanawake ambalo limewekwa kupitia TPB. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukija kwenye mpango mwingine ambao umeanzishwa na Serikali ni uanzishwaji wa jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi nawapongeza sana dhamira ni njema lakini hatujui bado jukwaa hili kwa kiasi gani litaweza kuwafikia wanawake wote Tanzania na kuweza kuwezesha ili tuone uchumi wetu unazidi kupaa kwa kasi kabisa. Kama amabvyo nimesema benki ya TPB ambayo tuna dirisha ya wanawake bado kuna umuhimu wa kuonyesha kwamba benki hii itawafikiaje wananchi wanaoishi vijijini kwa sababu lengo si kuwasaidia wanawake walioko mijini tu uwezeshaji wa wanawakekiuchumi ni kwa watanzania wanawake wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukija kwenye suala la asilimia nne ya vijana; asilimia nne ya akina mama na asilimia mbili inayoenda kwa watu wenye ulemavu katika Halmashauri zetu hii bado ni changamoto kwa sababu ile asilimi nne inaenda kwenye vikundi maalum, kwa hiyo hitaji la mwanamke kama mwanamke na familia yake bado haijafikiwa kwa lengo lililokusudiwa, watapata mahitaji kwa kiasi cha chini, mahitaji madogo kama ya chakula kwa hiyo si mbaya lakini tuzidi kuiboresha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nilikuwa nataka nijue hii asilimia mbili ambayo inaenda kwa wenzetu wenye ulemavu hawa hawana makundi, lakini kuna walemavu wenye ngozi na waliokuwa hawaoni, kuna ambao walemavu wa masikio, wako kila aina sasa sijui utekelezaji wake unakuwaje labda Mheshimiwa Waziri utakapokuja utuoneshe namna gani asilimia mbili hii inayoenda kwa wenzetu wenye ulemavu inatekelezwa na inawafikia na labda faida zake zilizopatikana mpaka sasa hivi katika hiyo asilimia mbili ambayo inaenda labda itapatikana vipi faida katika hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kwa heshima zote nimeamua kusudia kuweka kwenye eneo hili la uwezeshaji wa wanawake kiuchumi kwa sababu nina sababu nyingi sana, wanawake Tanzania tuko wengi, wanawake Tanzania tunajiweza kwa mambo mengi, kwa hiyo tunapopata fursa ya uchumi katika nchi hii Mheshimiwa Mpango na mipango yako mizuri uliyonayo basi uchumi wa Tanzania utakwenda kwa kasi kuliko hiyo ambayo umefikiria. Kwa hiyo mimi nasema hili kwa maana ya kwamba nina sababu za msingi, mwanamke anapojiweza kiuchumi familia yake inaimarika, hatokubali mtoto asiende shule, ataelimisha kwa kadri ya uwezo wa mtoto kusoma. Lakini pia lishe ya nyumba itakuwa safi ya baba na watoto, pia afya itakuwa imezidi kuimarika katika familia tutapunguza matatizo mengi yaliyo changamoto katika Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utekelezwaji wa watoto litapotea itakuwa si changamoto tena, mwanamke anajiweza kiuchumi, wewe mtelekeze yeye anaendelea na shughuli zake. Kwa hiyo jamani kuwezeshwa mwanamke kiuchumi ni jambo la msingi kabisa katika Taifa letu. (Makofi)

Naona wanawake tumefurahi lakini ndio ukweli ulivyo hivyo kwamba wanawake Tanzania Mheshimiwa Waziri Mkuu unanisikia ikiwa tutawezeshwa vizuri basi nakwambia uchumi wa nchi hii utapaa kwa namna ambayo ni ya ajabu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa wana baba nawaombeni tuna Mheshimiwa Rais wetu mpendwa kabisa ambaye anajaribu kuweka njia ya kuinyoosha Tanzania tuelekee kule ambako tunakutaka na mimi naomba aendelee hivyo nashukuru sana Mwenyezi Mungu ametuletea kiumbe ambaye anajaribu kunyoosha pale tulipopinda. Kwa hiyo, naomba Mungu atujalie tuendelee hivyo kwa hiyo lakini turudi siharibu hebu niacheni.

Sasa naomba nirudi kule kwa sababu kama hili ambavyo anatunyoosha kuelekea kwenye mambao mazuri tunayoyataka na wanawake atunyooshee tuendelee hivyo hivyo tutafika pahala pazuri sana Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Mipango. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli mpango huu ambao nimeusoma baada ya kutoka kwenye ajenda yangu hiyo, huu mpango mimi wala sina pingamizi nao najua kazi unayofanya ni nzuri na hii kazi ni nzuri zaidi kwa sababu pembeni yako kuna mwana mama hapo ambaye yuko vizuri, ana upendo, ana huruma na yuko makini sana hapo, kwa
hiyo haya mambo yanakwenda vizuri mimi naamini Wizara zikiwa na mama na baba mambo yatakwenda vizuri kabisa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naendelea kusema kwamba huu mpango kwa kweli naomba niwaambie Watanzania najua lazima mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni kazi zinazofanywa sio mbaya na tusiwadanganye Watanzania si kila jambo litakalofanywa na Serikali litawanufaisha watu wote ndege zinapoboreshwa Tanzania, watakaonufaika wapo na ambao watakuwa hawajui faida yake wapo lakini wakiwa wanufika si wananufaika katika nchi hii. Kwa hiyo sasa leo ndege yetu inakwenda China wafanyabiashara wataacha Ethiopian Airline, wataacha Kenya Airways, watapanda ndege yetu ya Tanzania watakwenda kufanya biashara zao kwa hiyo na mambo mengine mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaboresha umeme ukawa umeme mzuri zaidi tutafaidika na viwanda ambavyo tunavipigania, yote ni sahihi tuna changamoto, changamoto ni sehemu ya maisha, hizi changamoto ambazo amesema hapa Mheshimiwa Mpango ziko dunia nzima. Kwa hiyo hayo sio tatizo lakini na conflict (migogoro) katika dunia ipo sehemu zote kuna migogoro ya kisiasa, kuna migogoro ya kiuchumi, muhimu ni namna gani ya control ile migogoro isilete madhara katika dunia. Kwa hiyo, hayo naomba tuweke umakini sana.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala langu ambalo nimelizungumzia huu mpango huu pamoja na uzuri wake wote suala la uwezeshaji wanawake kiuchumi ndio mpango mzima, kama nilivyosema kwamba hii mipango ni mizuri sana lakini sekta tukimuweka mwanamke akawezeshwa basi mipango yote hii imeshamalizika haina jambo jingine ambalo litakuwa la ziada.