Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kidogo. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti kwa hiyo mambo mengi nimeyachangia huko sasa nataka kusema mambo machache tu madogo.

Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi anayofanya na aendelee, niseme tu kwamba nchi inayojenga uchumi na hasa uchumi wa viwanda kuna mambo kama sita ya msingi ambayo yanatakiwa iyafanye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni kujenga miundombinu ambayo ita-support uchumi huu ambalo Serikali inalifanya vizuri, lakini mazingira ya biashara ya kufanyia kazi na kuwekeza ni jambo muhimu pia. Jambo la tatu ni upatikanaji wa mitaji mikubwa ku-support miradi hiyo na mitaji hii inatoka nje na mingine iko ndani, jambo la nne ni ujenzi wa viwanda mama kama vya chuma, industrial evolutional ya Ulaya ilitokea kwa sababu walijenga viwanda vya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tano ni kuongeza matumizi ya malighafi za ndani tumesikia hapa wananchi wa Bunge wanasema kwa nguvu sana mazao ya kilimo yatumike hapa ndani, kuna mazao ya madini tuyatumie hapa ndani, tu-add value kwenye bidhaa tulizonazo hapa ndani. Na jambo jingine kubwa la mwisho ni matumizi ya teknolojia na wataalam, mafundi mchundo ndio wanaoweza ku-support jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kidogo sasa kwenye mambo hayo kadri muda utakavyokuwa kutoa ushauri kidogo. Kwenye suala la miundombinu naona mpango unapendekeza vizuri na unafanya vizuri tunaona barabara zinajengwa, reli inajengwa, miundombinu ya bandari inajengwa mambo haya ni muhimu umeme. Lakini kuna changamoto kidogo ambazo zinajitokeza na Wabunge wanasema, kwa mfano kwenye ujenzi wa reli tunafanya vizuri sana, lakini changamoto tuliyonayo ambayo nafikiri Serikali inatakiwa iangalie ni namna jinsi ambavyo tunaweza kupata fedha za kutosha kujenga hii reli kwa haraka, tunapojenga vipande kwa kweli tunaweza tukachelewa, tunaweza tukafika mwisho 2025 hatujafika kule ambako kuna mizigo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Serikali na Wabunge wengine wamesema tutengeneze huu mradi mmoja mkubwa kama tunaweza na tukope kwa concession kama inawezekana ni vizuri Serikali mkaendelea kuliangalia jambo hili kwa sababu tukiendelea kutafuta hela kidogo namna hii tunaweza kuchelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni lazima tuendelee kupanua miundombinu ya ndani barabara najua tunafaya vizuri lakini tuongeze juhudi. Kwa mfano kuna barabara moja kule mikoa ya kanda ya ziwa kule inayounganisha mikoa zaidi ya mitano ambayo inapita kwenye sehemu za kilimo cha pamba, barabara hii inapita kwenye kilimo cha mpunga, kwenye mifugo kwenye mazao ya misitu na inaunganisha vipande vingi sana vya shughuli za kilimo. Barabara hii inatoka Korandoto kwenye barabara inayotoka Shinyanga kwenda Mwanza na inapita Ukenyenge kwenye Jimbo hili la Kishapu kwa Mbunge sharp inaingia Jimbo la Igunga inaenda Jimbo la Igalula ikitoka hapo inaenda mpaka Tura inaunganisha barabara kutoka Dodoma kwenda Tabora.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inapita kwenye maeneo makubwa sana ya uchumi, naomba sana mpango huu kama inawezekana Mheshimiwa Mpango muiweke kwenye mpango, itasaidia sana kilimo cha pamba hata ule mkakati wa C to C (cotton to clothing) tunaweza kuutekeleza vizuri zaidi naomba sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili mazingira bora ya kufanyia biashara ni jambo ambalo limesemwa vizuri sana kwenye mpango, lakini bado kuna changamoto, wafanyabiashara na wajenzi wa viwanda wanahangaika wanapiga kelele kwa kweli, mahusiano kati yao na watendaji ni shida, wote mmesikia TRA mpaka Mheshimiwa Rais mwenyewe akasema TRA msiwe polisi sana, naomba jambo hili tuliendeleze tuhakikishe ushirikiano huu usiwe wa kipolisi na raia uwe wa partner, partnership ni muhimu.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona muda unakwenda jambo la pili ni mitaji kutoka nje na ndani, mitaji mikubwa ni lazima hii tuihamasishe, mazingira ya kufanya biashara wawekezaji kutoka nje tuwahamasishe waje, najua Serikali mmetengeneza blue print basi muitekeleze, mazungumzo na wenzetu hawa wanaowekeza kutoka nje myaendeleze na muwe marafiki zaidi, tusiwaone wawekezaji kutoka nje mara nyingi nimesema kama wanyang’anyi na wezi hapana, hawa ni wadau wetu, watatuletea fedha, tutafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni ujenzi wa viwanda mama kama nilivyosema Mchuchuma na Liganga ni project ambayo ni mama kweli tukipata chuma leo kwa kweli tutatoka haraka kabisa, bahati mbaya mradi huu umesuasua miaka mingi, kila mwaka maneno ni yale yale. Kamati tumesema jamani huu mradi sasa ufike mwisho, tukipata chuma tukapeleka kwenye viwanda vyote vya nondo na vya misumali tukatumia chuma kujenga reli yetu, majengo haya makubwa tukatumia chuma ya ndani tumetoka kiuchumi vinginevyo tuna kazi kubwa sana tutachelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ni kuhusu teknolojia, matumizi ya teknolojia na watalaam, kwenye mpango Mheshimiwa Mpango umesema vizuri sana, kada maalum za taaluma mnaziendeleza lakini juhudi hazionekani ni lazima VETA hizi tuzipe fedha ya kutosha, tuwapate hawa wataalam na mafundi mchundo wa kwenda kwenye viwanda vyetu, bila kufanya hivyo nchi ya India kwa mfano waliwekeza sana kwenye hiyo shughuli au shule za kuwafundisha mambo haya ya ufundi na wameweza sana kuendeleza viwanda vyao na sisi tunatakiwa tufanye jambo hili kwa nguvu nyingi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwa kusema...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mungu atusaidie, ahsante.