Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kwanza kukushukuru kwa kuniruhusu kusimama hapa na kama si jitihada zako baada ya Mwenyezi Mungu kuniruhusu, nitakuwa sijakufanyia haki lakini nikushauri tu na nikuombe, tunapoomba Mwongozo ungejaribu kutusikiliza kuna nini wewe ndio Mwenyekiti na unatoa ruling. Kuliwahi kutokea moto humu ndani wa simu, pengine lilikuwa jambo la hatari huwezi kujua, usidharau wito, dharau unaloitiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi asubuhi, katika kipindi cha maswali na majibu nilitetea Kampuni karibu mara sita na Naibu Waziri akajibu alivyojua mwenyewe, lakini yule jamaa sasa hivi ni mgonjwa ka-paralyze na yote hii kutokana na mazoezi ya kupanda ngazi na kushuka kwenye Maofisi. Anafanyishwa mazoezi bila kutaka mwisho wake kapata mtihani, kwa hiyo niombe Serikali hili suala iliangalie katika madeni na huyu umuangalie na Hansard zipo haya sio maneno yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye ukurasa wa 3 na 17 naomba uangalie maana nisijefika mahali nikawa nazungumza labda kitu sio. Niangalie kwenye hiki kitabu ukurasa wa 3 na 17 angalia halafu kama nitakosea nikosowe wewe ni mwalimu mzuri wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulihakikishia Bunge lako tukufu kwa ushauri, maoni yatakayotoka katika kikao hiki cha Bunge yatazingatiwa kikamilifu katika kuandaa rasimu ya mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, humu naomba kuisoma hii Hansard na juzi ulikuwepo tena ili iwe record katika Bunge hili nitakapokuja kufa angalau historia itanihukumu au itanikumbuka; “Sasa kwa sababu ahadi ilikuwa ni Bunge hili basi, tutasogeza ahadi kwa Bunge lijalo, Bunge lijalo halipo mbali sana, kwa hiyo ni vizuri kwa kweli mtakapotoka hapa basi mjitahidi Bunge lijalo tusikie lugha nyingine ili tuendelee na mambo mengine, tunajua ni kubwa na lina mambo mengi, lakini umuhimu kwa sababu ya interest kubwa ya zaidi ya Muungano.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa wa 17 miradi ya umeme. Utekelezaji wa miradi ya umeme na kufufua kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya nishati ikiwemo maji na gesi, kuendeleza miradi ya umeme ikiwemo sakata hili la Zanzibar la VAT umeme mara mbili, na sheria ya VAT mradi wa mwisho unaotakiwa alipe VAT ile hili sakata la muda mrefu.

Kwa hiyo imefika mahali hili Bunge na haya maneno ni mazito katika chombo hiki, lilifika hili suala Serikali itoe kauli, tulishaambiwa Bunge linalokuja, linakuja linakwenda, linarudi tunafika wapi? Kwa hiyo, hili suala liangaliwe, Mheshimiwa Waziri nilishajitahidi sana kumfuata anavyotaka yeye na Mwenyezi Mungu shahidi, nilishampa mpaka viongozi wakuu si vizuri kuwataja hapa kuzungumza nao hili suala linatusokota, hatutendewi haki na si suala hili tu la VAT la umeme bidhaa yoyote iliyotoka Tanzania Bara ikaingia Zanzibar VAT mara mbili. Nini maana ya VAT, nini formula yake tupeni definition ya VAT. Imekuwa tunasokotana tu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitabu cha mapendekezo ya mpango wa maendeleo ya Taifa kujumuisha mapitio ya hali ya uchumi, utekelezaji mipango na maendeleo ya mwaka 2017/2018 robo ya kwanza ya mwaka 2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa uchumi ikiwemo mabenki uchumi, leo FNB Bank ina mwaka wa tatu, watu wanateseka tumeuliza kwenye chombo hiki mara nne, mimi mwenyewe mara mbili, tumefanya semina na watu wa Benki Kuu humu ndani wakatuambia muda si mfupi pesa zitapatikana wengine wameshatangulia mbele ya haki kwa Mwenyezi Mungu, sasa huku wanataka kuhujumu uchumi pesa zimebaki tu kule, na pesa dhamana ni Waziri wa Fedha kupitia Benki Kuu, hebu toeni ufafanuzi hizi pesa na sio kama benki imefilisika, pesa ziko wapi, Dutch Bank ya Ujerumani. Tunaambiwa zinaletwa, zinaletwa kwa mguu au kwa baiskeli na hazifiki mpaka leo, wananchi wanaumia Serikali ndio wananchi na wananchi ndio Serikali, hebu fikeni mahali mliamue hili suala.

Lakini jambo lingine wafanyabiashara wadogo wadogo wa Zanzibar wenye hata tv moja, simu tatu za mkononi wakafika Bandarini Dar es Salaam wanapata fatiki, wananyanyaswa na hesabu inaanzia moja hata hao matajiri wakubwa walianza na hesabu hii moja, wakafika mbili, wakafika tatu. Mtoto akizaliwa haendi mbio siku hiyo hiyo, hutambaa akaokotwa, akaanguka, akakamata ukuta. Sasa mfike mahali wafanyabiashara wadogo muwathamini. Bandarini Dar es Salaam kumekuwa usumbufu maana utafikiri unakwenda wapi, hakuna mvua, hakuna jua, hakuna usiku, hakuna mchana. Tufike mahali Waziri wa Fedha uwaonee huruma, na wao wanataka kupanda V8 hawa. Eeh hesabu inaanzia moja, mtoto hazaliwi akaacha ziwa siku hiyo hiyo. (Kicheko)

Mheshimwa Mwenyekiti, nije habari ya viwanda ukurasa wa 42 kama sikosei katika kitabu hiki maana itabidi twende kwa data sasa hivi. No! no! naomba Hansard ikae sawa 42 kuhusu udhibiti wa matumizi ya fedha za umma sio viwanda, matumizi ya fedha za umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar niipongeze sana Benki Kuu sana unajua tuseme ukweli penye ukweli tuseme ukweli katika watu wanaolipa kwa wakati 4.5 Benki Kuu, hili niwapongeze sana Waziri wa Fedha nakutuma unipelekee salamu kwa Gavana hili lazima tushukuru. Lakini hii 4.5 toka urembo ungali tunguja wazee wetu walikuwa wakijifunga vile vitu vya ajabu ajabu kwenye masikio sasa hivi dunia imekuwa, population ya Zanzibar imekuwa 4.5 hii haikidhi, ifike mahali izingatiwe barabara zimeongezaka, watu wameongezeka, vituo vya afya vimeongezeka, population imekuwa. 4.5 imepitwa na wakati, kwa hiyo, mfike mahali mzingatie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanda vya Zanzibar. Nadhani itakuwa kengele ya kwanza kama sikosei.