Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kukushukuru kwa kunipa hii nafasi ya kuchangia Mapendekezo ya Mpango ya Taifa 2019/2020. (Makofi)

Kwanza nimpongeze kwanza Mheshimiwa Waziri Mpango na nimpongeze sana Mheshimiwa Rais na Serikali ya Awamu ya Tano, katika ujumla wake kwa kuwa consistency katika kipindi hiki chote cha miaka mitatu kwa sababu mpango huu ni sehemu ya mpango mzima wa miaka mitano 2015/2016 - 2020/2021 na katika utekelezaji wake Serikali imekuwa consistency sana.

Pia niipongeze Serikali kwa kuzingatia maoni ya Wabunge kwa miaka yote mitatu ambapo tumekuwa tunatekeleza mpano huu. Maeneo kadhaa ambayo tulikuwa tunashauri yakiwemo maeneo ya kuongeza nishati tumeona Stiegler’s Gorge imeendelea kupewa kipaumbele lazima tuipongeze lakini pia tumeona leo Liganga na Mchuchuma, inaanza kupata sura ya utekelezaji kwa maana kwenda sasa kujenga kiwanda cha kufua chuma Liganga. Sasa haya yote ni mapato ya kazi ya Bunge hili na nimatokeo ya kazi nzuri ya Awamu ya Tano, na lazima tuipongeze Serikali na kwa namna ya pekee Mheshimiwa Rais na Waziri Mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la kukua kwa uchumi wote tumejiridhisha pasipo mashaka uchumi wetu unakua kwa kasi kubwa sana na ukilinganisha na uchumi unavyokuwa duniani na uchumi unavyokuwa katika Afrika na maeneo mengine tunayopakana nayo sisi tunakuwa kwa kasi kubwa sana, kasi ya asilimia 7.2.

Sasa hili kimsingi kuna eneo dogo linatupa shida kidogo sisi Wabunge lakini Watanzania katika ujumla wake kwamba uchumi unakua, lakini mapato ya kukuwa uchumi huu tunayaona kwenye maeneo ya afya, tunaona kwenye masuala ya elimu, tunaona kwenye masuala ya miundombinu. Kwa hiyo, kimsingi faida za kukua uchumi huu tunaziona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ambayo mimi nilitaka nitoe mapendekezo, ya kuboresha wakati wa maandalizi ya huu mpango ni namna gani sasa kwa sababu mimi nina amini hatuwezi kupata mapinduzi ya uchumi kama hatutakuwa na mapinduzi ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilitaka nijaribu kushauri kwamba sasa Mheshimiwa Mpango akae na hizi line ministry zinazogusa sekta ya kilimo na uchumi kiujumla kuona namna gani sasa tunaweza ku-transform agricultural sector kwa namna ni significant. Waatalam wa kilimo wanapo taka kujua changamoto kwenye sekta ya kilimo wanafanya upembuzi wa mnyororo wa thamani ya mazao ya kilimo na ukifanya upembuzi wa mnyororo wa thamani wa mazao ya kilimo katika ujumla wake utagundua kwamba tatizo kubwa kwenye sekta ya kilimo ni soko, yaani huo ndiyo mtego tunao na Serikali sasa lazima ikubali kwamba huo ndiyo mtego ambao tunao na tukiweza kuutegua huo sekta ya kilimo itakuwa kwa kasi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye huu mpango nashukuru Serikali imeweka vizuri sana interventions nyingi kwenye sekta ya kilimo, lakini utaona kwenye interventions zilizopendekezwa na Serikali kwenye mpango huu hazioneshi kwa ufasaha namna gani tunaenda tunaenda kutatua tatizo la soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachomfanya mkulima aende shambani ni faida anayoipata kutokana na kilimo. Tumejiridhisha kwamba kwa namna yoyote ile kwa mazingira aliyopo mkulima huyu mdogo lazima achangie kwenye usalama wa chakula, lakini lazima atengeneze fedha kwa ajili ya kujikimu. Sasa strategy ya Serikali lazima izingatie ukweli kwamba kumsaidia huyu mkulima mdogo apunguze gharama za uzalishaji na gharama za uzalishaji kwanza zinatokana na bei kubwa ya mbolea, nashukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu jana alieleza namna gani tunajipanga kupunguza gharama ya mbolea kwa kuzalisha mbolea yetu ndani, hilo litamaliza tatizo lakini kwenye mpango huu alijafafanuliwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini eneo la pili ni transaction cost kutoka eneo lile ulilozalisha mpaka kufika kwenye maghala ya kuhifadhia mazao, barabara zetu vijijini hazileti tija kwa mzalishaji, eneo dogo la usafirishaji analipa gharama kubwa sana za kusafirisha mazao yake,
anapofikisha zao lake kwenye eneo la soko tayari garama imeshakuwa kubwa. Kwa hiyo anapokutana na bei ndogo, profit margin inabaki kuwa ndogo sana au anaweza asiipate kabisa. Kwa hiyo, Serikali iwekeze kwenye kupunguza gharama za uzalishaji kwa kupitia pembejeo zetu, mbegu bora na mbolea, lakini pia miundombinu ya masoko, na miundombinu ya masoko ndiyo hizo barabara za vijijini zinatoka mashambani lakini madaraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine baya linalochangia upotevu mkubwa wa mazao tunasema post harvet losses ni haya hadhi na sura ya maghala yetu na gharama za usafirishaji (miundombinu ya usafirishaji) asilimia 30 ya mazao yetu tunayoyazalisha yanapotea kabla hayajafika kwenye soko, sasa hiki kiwango kinacho potea nacho ni hasara kwa mkulima. Kwa hiyo pamoja kwamba hatuwezi kumsaidia mkulima kupata bei nzuri kutokana na hali halisi ya soko la dunia tunaweza kama Serikali kumwezesha huyu kuzalisha kwa gharama za chini na hii profit margin yake ikabaki kubwa na akawa ana visenti vya kwenda shambani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliomba nimshauri Mheshimiwa Mpango na Serikali katika ujumla wake katika eneo hilo na ninakushukuru sana na ninaunga mkono hoja, ahsante.