Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kitu kinachoonyesha Serikali hii kwa kupanga tuu inajua kupanga, lakini kwenye kutekeleza, ipo shida, mipango ipo mingi lakini utekelezaji ni shida sana sana. (Makofi)

Kwanza ningeanza kuongelea suala la nishati. Tulikuwa na mradi wa nishati kwa kutumia gesi, mradi huo ambao bahadhi ya ndugu zetu ndugu zangu wa Kusini (Mtwara na Lindi) waliandamana na hata tulipoteza baadhi ya ndugu zetu na wengine walifunguliwa kesi, wengine walikimbia nchi kwa ajili ya huo mradi. Mradi huu ulitumia takribani hata zaidi ya trilion 1.2; lakini pia wananchi walilazimika kuacha makazi yao, mashamba yao na kushindwa kuendelea na kazi kwa ajili ya kujiinua kiuchumi na mpaka leo hii baadhi yao hawajalipwa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunaona Serikali ya Awamu ya Tano inaenda kuua ule mradi wa gesi, imekuja na mradi mpya wa Stieger’s Gorge. Mradi huu ambao kwanza kwa taarifa tuliyopewa utaenda kugharimu pesa nyingi zaidi kuliko ule mradi wa gesi, tumeambiwa mpaka kumalizika huo mradi inaweza ikatumika takribani trilioni saba na hadi sasa zimetengwa, bilioni 700 kwa maana hiyo hadi kuja kumalizika itakuwa ni ndani ya miaka kumi, kwenye hatua za awali tu tayari imetumika bilioni 700.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi najiuliza, huu mradi kuna kitu gani mpaka tunalazimishia uendelee pamoja na kwamba wataalam wametuambia kuna athari nyingi zitakazoenda kujitokeza kwenye mazingira, lakini bado tunataka kuendeleza na huu mradi, tuna option nyingi za kuweza kwenda nazo, kwanza kuna hiyo gesi ambayo tayari tumeshatumia fedha, lakini pia vilevile kuna upepo, kwa sababu huu mradi wa Stieger’s Gorge kama ni megawatts umeme utakaoweza kuzalishwa ni megawatts 2,100 ukiangalia mradi wa upepo unauwezo wa kuzalisha umeme wa megawatts mara nne na zaidi wa huu hapa wa Stieger’s Gorge kwani kuna kitu gani hasa kwenye huu mradi wa Stieger’s Gorge tunahitaji kujua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakumbuka vizuri kabisa, wakati tupo kwenye kipindi cha Bunge la Bajeti, Waziri wa Mazingira, Mheshimiwa Januari Makamba, Serikali itakuja kufanya tafiti kujua hizo athari, lakini cha kushangaza wenye hili hapa huu mpango tunachokiona hakuna pesa yoyote iliyotengwa kwa ajili ya kufanya hizo tafiti juu ya hizo athari zinazoweza kujitokeza. (Makofi)

Sasa na juzi tumemsikia kabisa Rais Magufuli akisema kwamba huu mradi utaendelea kufanyika na ametupilia mbali zile information ambazo zipo bian stone research. Sasa tunataka kujua tunaendea na huu mradi kwa research gani ilifanyika na Serikali? Kama kuna research imefanyika basi tulitewa tuweze kujadili hapa ndani Bungeni. Kwa sababu sielewi kwa nini tunaendeleza kitu ambacho kwa asilimia kubwa itatuletea sisi wenyewe athari nyingi, na ukikaa ukiangalia huu mradi there is no sustainability kwa sababu kama ni maji, maji yatafika wakati yatakwenda kuisha, kwa sababu maji yanatumika na wanyama, mimea, binadamu wote tunategemea kutumia haya maji. Kwa hiyo ikifika sehemu maji yameisha tunafanyaje?