Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii kuchangia Mpango wa 2019/2020. Nianze kwa kuwapongeza kuwa huu mpango ni mpango mzuri sana ambao kila mmoja kwa kweli ana uangalia na inabidi ajivunie kwa sababu ni mpango mzuri. Jambo ambalo naomba kuongelea naomba nishauri kuwa miradi ambayo imeshaanzishwa hasa kwa muda mrefu naomba sana iangaliwe kwenye vizuri kwenye Mpango huu, kwa mfano huu mpango wa Mchuchuma na Liganga uweze kumalizika na kuangaliwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba kushauri kwenye maendeleo ambayo yapo maboma wananchi wengi wamejenga maboma ya shule, maboma ya zahanati, maboma ya vituo vya afya na vyenyewe naomba viangaliwe kwenye mpango huu viweze kuhusishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni umeme, umeme ndio nashukuru na ninapongeza Serikali, nampongeza Mheshimiwa Rais anafanya vizuri sana, lakini kuna vijiji pamoja na vitongoji ambavyo bado havijapata umeme kwa hiyo ningeliomba viweze kuangaliwa kwenye mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naomba kuangaliwa kwenye Mpango huu, ni maji, maji ni muhimu sana, unakuta kweli Wizara ya Maji inafanya vizuri sana lakini kila mmoja ananikubalia kuwa licha ya kufanya vizuri bado kuna matatizo ya maji kwenye sehemu mbalimbali, kwa hiyo naomba sana hili jambo liangaliwe hata kwenye Kata yangu ya Magadu bado tuna tatizo la maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naomba liangaliwe ni kwenye mikopo ya elimu ya juu. Naomba sana vigezo viangaliwe kusudi wanafunzi wengi waweze kupata mikopo, kwa sababu unakuta amefaulu lakini hakujaliwa kupata mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ninaloongelea ni kilimo, kilimo kinaajiri zaidi ya watu zaidi ya 65.5% na asilimia 100 ya chakula kinatoka kwenye kilimo, lakini tunafanya vizuri ndio kwenye kilimo, lakini bado hatujapata kipaumbele kabisa kwenye upande wa bajeti naomba sana, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango uangalie kuwa kuna tulikubaliana kwenye Malabo kuwa ni 10% kwa hiyo tuangalie kuwa itakuwaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye upande wa utafiti hatuwezi kuendelea bila ya utafiti, kwa hiyo tutenge hela za kutosha kwenye mpango huu tuone kuwa utafiti utakwendaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye upande wa pembejeo uzalishwaji wa mbegu nashauri na naomba mpango uwepo wa kuzalisha mbegu hapa nchini, yaani tuzalishe sana hapa nchini kuliko kuchukua mbegu za nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naomba kuongelea kwenye kilimo, ni viwanda vya kuzalisha mbolea, ndio vimeanza lakini bado havijachukua kasi, kwa hiyo, kwenye mpango huu, licha ya kuwa na mbolea inayoingia kutoka nje, lakini naamini kuwa tukizalisha kwenye viwanda vyetu hapa Tanzania mbolea itakuwa chini na wakulima wengi wataweza kuinunua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni viwanda vya dawa za wadudu, yaani viwatilifu, nashauri kuwa tuwe na viwanda, mpaka sasa hivi tuna kiwanda kwa wastani kimoja ambacho kiko Njombe (Mafinga) cha Pareto naomba sana,.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tuwe na viwanda vingi, naomba niongelee uvuvi, uvuvi bado hatujaendelea vizuri kwenye uvuvi wa bahari kuu, naomba sana tujikite kwenye mpango wetu huu kuangalia jinsi tukavyoendeleza uvuvi wa bahari kuu na yenyewe tukazie sana kwenye mpango huu ununuzi wa meli ili tuweze kuwa na meli zetu za uvuvi kwenye bahari kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, ni ujenzi wa bandari ya uvuvi, niko kwenye uvuvi, tuweze kuwa na bandari ya uvuvi, kusudi tuweze kuvua samaki ambao wanatoka kwenye bahari kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, cherezo, tukiwa na meli tuweze kuwa cherezo yetu, ambayo imejengwa hapa nchini kusudi meli zetu ambazo tutanunua kwenye mpango huu, ziweze kutengenezwa na kukarabatiwa kwenye nchi yetu badala ya kwenda Mombasa na nchi nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tuwe na viwanda, mpaka sasa hatuna viwanda vya kuchakata samaki, hasa wa bahari kuu, kwa hiyo naomba tuweze kuwa na mpango uweze kuhusisha viwanda vya kuchakata samaki bahari Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa mifugo, mifugo tuweze kuwa na mpango ambao utahusisha kuwa na ufugaji wa kisasa, sio ufugaji wa kuhamahama na hasa tuki-focus sana kwenye malisho, uwepo mpango wa kwenye malisho pamoja na mpango wa kwenye viwanda, pamoja na mpango wa kwenye mambo ya miundombinu, nikisema miundombinu namaanisha ujenzi wa mabwawa pamoja na majosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine naongelea kwenye upande wa mazingira, mazingira yetu mpaka sasa hivi, hayafurahishi kwa hiyo naomba sana, mpango wetu huu, uweze kuhusisha mambo ya mazingira. Kwenye mpango huu wa 2019/2020 mipango iliyopita imeonesha changamoto, naomba kwenye mpango huu ambao tunakwenda nao wa 2019/2020 tuweze kuona jinsi ya kutatua hii changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.