Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi naomba niunge mkono Kambi Rasmi ya Upinzani maana na sisi tumetoa dira, mwelekeo na mpango ambao tunafikiri Serikali mnaweza mkaufuata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwanza nataka nizungumzie kilimo. Tunapozungumzia kilimo ambayo tukimechukua asilimia takribani 75 ya Watanzania wamejikita katika kilimo, lakini katika mpango huu ambao Mheshimiwa Mpango umeuleta hatuoni nguvu ya Serikali kusaidia wakulima wa Tanzania waweze kukuza uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ambazo tumekuwa tukipanga Wizara inatoa asilimia mbili tu ya mapato kusaidia wakulima. Tunafahamu kwamba katika kilimo usipoweka pesa wewe kama Serikali na ukitegemea wafadhili wakupatie pesa kwa ajili ya kilimo na bahati mbaya sana wafadhili wenyewe mmeanza kuwakorofisha. EU iliahidi kutoa hela zaidi ya bilioni 200 kwa ajili ya kusaidia kilimo tayari tumeanza kukorofishana nao sijui tutafika wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo kwa Nyanda za Juu Kusini niachilie mikoa mingine hakuna dalili zozote za kusaidia hasa katika tafiti ili uwe na kilimo bora kwanza kabisa lazima ufanye tafiti. Mwalimu Nyerere alijitahidi kuweka vyuo mbalimbali vya kilimo ikiwemo Chuo cha Uyole mpaka sasa zaidi ya miaka mitano hawajawahi kupata pesa za maendeleo kwa ajili ya chuo kile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna viwanda vingi vilianzishwa ili viweze kusaidia wakulima kwa mfano ZZK walikuwa wakitengeneza zana za kilimo ikawa rahisi kuwafikia wananchi kwa ngazi ya chini, leo hii kila kitu tunatoa nje, tunatoa China kwa gharama za kigeni kuweza kuwafikia wakulima mwisho wa siku pembejeo zinakuwa ni bei kubwa sana kuwafikia wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbegu ambazo ndio zinatakiwa zizalishe chakula cha Watanzania asilimia 90 ya mbegu tunaagiza kutoka nje. Bahati mbaya sana mbegu nyingine zimekuwa sio rafiki kwa ardhi ya kitanzania ndio maana ninarudi nyuma kwamba tunahitaji kuwa na watu wanaofanya research ambao watajua mbegu hii inafaa kwa ardhi hii au zao hili linafaa mkoa fulani na watu hawa waweze kusaidia wakulima waweze kupata mazao yanayostahiki.
(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia connection ya Wizara tofauti ili kuweza kusaidia Wizara mama kuwa na mafanikio sisi kama watanzania tumeshindwa. Leo hii watu wanaohusika na mambo ya hali ya hewa hawawezi kufanya kazi kwa karibu sana na Wizara ya Kilimo kuweza kujua mwaka huu tunalima mazao kadhaa kwa kupata taarifa kutoka kwa wataalam, kila mtu anafanya kazi anavyoona yeye inafaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maji na Wizara ya Kilimo; maji na kilimo vinaenda sambamba, lakini wasipofanya kazi kwa pamoja Wizara ya Maji haina pesa, Wizara ya Kilimo haina watafiti, tunawezaje kufanikiwa katika kilimo na tunawezaje kuwa na maendeleo ya kiuchumi kama Watanzania na kuwafanya wakulima wanapata mazao kwa wakati sawasawa na ubora tunaoutaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mashirika mbalimbali yakisaidia upatikanaji wa mbegu. Kama mnakumbuka Ukiliguru zamani walikuwa wanashughulika na mambo ya mbegu, sasa hivi watu kama wale wako wapi? CCM mlikuwa na kitu kinaitwa SUKITA kiko wapi? Vitu mbalimbali vilikuwepo zamani kwa ajili ya kusaidia wakulima hawapo, havipo na wala hakuna ubunifu wa kuanzisha vitu vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie habari ya utawala bora na ukuaji wa uchumi. Usipokuwa na utawala bora na umoja na wananchi kutoka ngazi ya chini mpaka Taifa mnakosa nguvu na moyo wa watanzania kufanya kazi ili kuweza kuleta maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wengi wamezungumza mahali hapa kuhusu Katiba Mpya na hii ipo katika mpango ambao sisi tumekuwa tukiuzungumzia. Huwezi kuwa na maendeleo yoyote kama hamjajiwekea utaratibu wa utawala. Watu walitoa pesa (kodi) tukaweka Tume, wakazunguka nchi nzima, wakaweka utaratibu wa kuweza kuona kama Watanzania tunaishije, leo hii tumeacha na kuishia pembeni, kwa maana pesa zote zilizotengwa zimekwishakupotea ambayo ilikuwa ni kodi ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba utakaporudi utueleze umepanga nini na ni kwa nini Serikali yako inakataa kuzungumzia Katiba Mpya ili twende kwenye mustakabali wa maendeleo yetu hapo baadae. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi na usalama ni kitu cha muhimu sana katika Taifa letu la Tanzania. Usipokuwa na ulinzi na usalama wawekezaji wanaondoka. Tumekuwa tukisikia mambo mengi yakitokea na sisi kama wananchi na hata kama Wabunge hatujapata taarifa ya kueleza kwa nini wawekezaji wanatekwa na wanafukuzwa na kama wamekosea je, mmefanya njia gani mbadala mpya ya kuweza kuwatangazia utaratibu mpya wa kuwekeza ili watu wasiwe na mashaka na ulinzi wa Tanzania na usalama wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pasipo na usalama hakuna mtu atakuwa tayari kuja kujiunga na Watanzania. Tupo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, watu wanaona ni bora wahamishe bidhaa zao kwenda Kenya, Uganda na sehemu zingine kuliko kuja sehemu ambayo haina uhakika wa ulinzi wa maisha, mali na mitaji yao watakayowekeza. Tunaomba unapokuja kutueleza Mheshimiwa Mpango ueleze Watanzania pamoja na sisi Wabunge ni mkakati gani umejiwekea wa usalama wa wawekezaji; utatumia njia gani ya kuwalinda hata hao wachache waliobaki waendelee kutumika katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda sana kutoa ushauri, vitu vingi sana vinavyofanyika sasa ambavyo vinaharibu kabisa umoja wetu na hasa katika maandalizi ya kutetea uchumi wa Taifa letu. Mimi ninaomba usimamie TRA ambao ni wakusanyaji wa kodi kwa kweli wamekuwa kama ni askari, hawana umoja na wafanyabiashara na sasa hivi imefika mahali hata wenye mitaji ya 300,000 wanahitaji kulipa kodi, ni kweli sikatai kwamba wasilipe kodi lakini lazima zitungwe sheria ambazo zinasaidiana kuweza kuwasaidia hawa watu wajione wana wajibu wa kufanya hiyo kazi ya kukusanya kodi pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na hali ya udhalilishaji mkubwa sana kwa wafanyabiashara na kumekuwa na matamko mengi hasa Wakuu wa Wilaya kufungia makoso kwa sababu za kisiasa. Wakati mwingine tuliona pale Tunduma, muda mrefu sana masoko yamefungwa, zile pesa ambazo siku ile hazikuingia Serikali ilikosa mapato sababu ya siasa. Vivyo hivyo Mbeya soko la SIDO lilifungwa kwa muda mrefu kwa sababu za kisiasa… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji