Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nitaanza kwa kum-quote anaitwa Authon, aliwahi kusema; “accuracy is the twin brother of honesty,” lakini Edward akasema; “accuracy of the statement is one of the first element of truth” au unazunguka unasema in accuracy is the near keen to falsehood, kwamba usipokuwa accurate you are likely to lie, usipokuwa na taarifa ambazo ziko sahihi, utasema uongo tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina-quote hotuba ya Kamati ambayo mimi ni Mjumbe wake, tumetoa mapendekezo mazuri, akasema ni; “ni muhimu pia ikaangalia kwa makini suala la watumishi wa Wizara na uwezo wao wa kufanya kazi kwa ueledi zaidi.”

Ninarudi kwenye ripoti ya CAG, yeye akasema tulikuwa/tumekuwa na issue kwa muda mrefu ya kutoonekana kwenye vitabu 1.5 trillion; alikuja kwenye kamati yetu na ametoa taarifa yake. Nina-quote sehemu ndogo anasema; however these re-worked totals did not fully reconcile as there where an excess of expenditure over revenue amounting to figure of 290.13 billion. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kumbe alienda kukagua authenticity ya 1.5 trilion akakuta kuna kitu kingine, kuna ongezeko la 290 bilioni. Kwa hiyo kwa jibu simple na alichoenda kuangalia kwamba wapi 1.5 trillion akakuta kuna kingine zaidi ya 1.5 trillion, akakuta kuna ku-spend zaidi kwa bilioni 290. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini tumefika hapa, ni kwa nini tumekuwa na hoja za ukaguzi? Ninarudi kwa watumishi wa Hazina ambao tunawategemea na hawafanyi kazi inayostahiki. Mjumbe yeyote wa Kamati akisimama hapa asiongelee suala la utendaji usioridhisha wa Hazina ambao umeleta hizi auditing queries. Kama tusipo-address hili suala litaendelea kujitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali najiuliza, ilikuwa ni bahati mbaya kwamba taarifa hazikuwasilishwa kwa wakati kwa ajili ya kukaguliwa na CAG? Ilikuwa ni bahati mbaya kwa wafanyakazi ambao wapo competent, kwa watu ambao wanajua nini…

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: …deadline ni lini ya kuwasilisha hesabu…

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Goodluck Mlinga.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia Theonest unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, sita-deal na watu wanaotafuta umaarufu mdogo mdogo, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeanza na quote yangu kuonesha weakness kubwa ambayo ipo Hazina ambayo ndio imepelekea kupotea kwa kiwango kikubwa cha fedha ambacho hata leo Mheshimiwa Catherine ametuweka wazi si tena 1.5 trillion bali ni two plus trillion. (Makofi) [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Khadija Nassir.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Khadija.

Mheshimiwa Anatropia Theonest.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nimesema utendaji wa Hazina, siamini kwamba ni wa bahati mbaya, ninaamini kwamba ni utendaji mbovu wa makusudi unaotupeleka au unaotufikisha hapa tulipo leo. Ninaongea kwa masikitiko kutoka kwenye executive summary ya CAG anasema wakati wa kutunza kumbukumbu zao katika…

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa…

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, tunaongelea Hazina ya Taifa inayotumia spread sheet katika kutunza taarifa.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, ina maana haya mambo yamefanywa deliberately, haya mambo yamefanywa kimkakati na tupo likely kuendelea kuona hayo mambo, tutakuwa na reconciliation leo, kesho na keshokutwa. Ni Hazina gani haijui lini mwisho wa kuwasilisha taarifa kwa ajili ya ukaguzi wa CAG? Kama haitoshi CAG pia ameanisha kwamba kumekuwepo na mismatch ya hundreds billions of money kutoka kwenye exchequer issue warranty. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano kuna exchequer issue warranty ya bilioni 656.5 ambazo exchequer issue warranty hazi-match na exchequer issue report. Tuna exchequer issue warranty za bilioni 3.45 ambazo zimekuwa cancelled na hakuna taarifa kokote kuonyesha zimekuwa cancelled. Pia kuna exchequer issue warranty ya bilioni 56.07, wameweza ku-verify only 51.3 billion ambayo kuna earning ya bilioni tano na ikaonyesha kwamba Wizara ili-cancel bilioni moja na hapo tunabaki na bilioni 3.29 hazijulikani taarifa zake zipo wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kama haitoshi, kuna exchequer warrant ambazo ni za shilingi bilioni 234. Kwenye Exchequer Release Report hazionekani kokote na wanavyoulizwa, nina-quote hapa, anasema: “The Ministry explained that the fund were released for the previous year transcations which were processed but would not be cleared in The Financial Year 2015/2016.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG akaenda mbali akasema: “The lack of disclosure records of the prior year transaction in the question indicates that the exchequer report was misstated.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako madudu mengi sana ambayo ukiyatazama sisi kama Wanakamati tunaamini kwamba ni lazima mfumo ufanyiwe overhaul. Tusipofanya hivyo, tutakuta fedha nyingi zimeibiwa kuliko ambavyo tunafikiria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikiongelea kuiba siyo lazima uzipeleke kwenye mfuko wako. Kama fedha zimekuwa planned kufanya kitu A na umefanya na hakuna detail au hakuna viambatanisho, kwa Mhasibu au kwa mtu yeyote anaye-deal na hesabu, hizo fedha zimepotea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakwenda kwenye suala la matumizi ya Fedha za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Kumekuwepo na ununuzi usioridhisha au uwekezaji usiokuwa na tija wa billions and billions of money. Mfano, ardhi iliyonunuliwa katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, ameeleza mwenzangu kwamba plots nne tu. Nimekwenda mbali zaidi, wanasema ni kama ekari 1,000, lakini fedha iliyotumika ni takribani shilingi bilioni 16 point something. Haiingii akilini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakaeleza hata eneo lingine liko Kigoma, Mwandiga, ekari moja kwa shilingi milioni 66. Haiingii akilini! Unaona kwamba kama Serikali ipo, kwa sababu mmeongea leo kana kwamba hii Serikali ndiyo kwanza ina mwaka wa tatu; hii Serikali tuliyonayo leo ina takribani miaka 56 plus madarakani. Kwa hiyo, haya madudu tunayoyaongelea leo yametokea miaka yote ambayo mmekuwa madarakani na ninyi ambao mnapaswa kuisimamia Serikali mnapaswa kuwa answerable. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeongea kwamba kuna fedha, shilingi milioni 888 wamelipwa watu ambao sio Askari Jeshi, sio Polisi, majina yao yapo yameainishwa na Mheshimiwa Waziri anayaona, Waziri ambaye anajitamba kwamba anafanya kazi. Mmeshindwa nini kuwafikisha kwenye vyombo vya dola, kama siyo kwamba tunalea watu na tunaonea watu ambao tunadhani tunaweza tukawaonea? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. In a nutshell nasema, tulichokiona katika Hazina ya Taifa ina-reflect nia yetu kama taifa, ina-reflect kwamba hayo makosa yaliyofanyika katika kuweka takwimu yamefanywa deliberately, kwa lengo la kupoteza au ku- misdirect fedha za walipa kodi. (Makofi)