Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyetufikisha hapa tulipo leo na Serikali ya Dkta John Pombe Magufuli mbele ya Watanzania inaendelea kuthibitisha kwamba ni safi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia na napenda sana kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kazi anazoendelea kuzifanya, nampongeza sana. Aendelee kukaza kamba, Watanzania wamemuelewa na sisi tutaendelea kutenda kwa ajili ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeanza kuyasema haya ili tuweze kuwa na uelewa wa pamoja kwa sababu yamesemwa hapa kulikuwa na Special Audit, hivi hata kusoma kawaida tu hatujui? Special Audit, nini kilichoandikwa ndani ya taarifa ya Mkaguzi Mkuu na nini kilichoandikwa ndani ya hotuba ya Mwenyekiti na Kamati yake? Mheshimiwa Mwenyekiti nikupongeze sana na Kamati yako kwa kuendelea kusimama imara, hukutikisika hata pale ulipotikiswa na ukahakikisha Watanzania wanakuwa na taarifa sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana wachangiaji wote waliochangia, nimshukuru sana Waziri wa Kilimo ile sehemu ya kwanza niliyotaka kuisema ameisema, sasa naomba niende kwenye sehemu ya pili. Tukichukua taarifa hii tukaisoma vizuri, hii ya Mwenyekiti wa Kamati na Kamati ya PAC, tunakwenda kwenye hadidu za rejea kwa nini CAG alitakiwa kufanya uhakiki (verification). Alitakiwa kufanya uhakiki huu na Bunge lako Tukufu kwa sababu, kwanza, siyo kwamba yeye alikuwa na hoja ya upotevu wa shilingi trilioni 1.5. Taarifa zake za mwanzo alizowasilisha mbele ya Mheshimiwa Rais, alizozikabidhi Bungeni hazikuwa na hiyo hoja lakini watu wasiolitakia mema Taifa hili, wasioitakia mema Serikali ya CCM ya Awamu ya Tano wakaja na hoja hii ya upotevu wa shilingi trilioni 1.5. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata Serikali tulipotoa kauli hapa tarehe 20 Aprili, bado waliendelea kusema na kwa sababu Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu, tulisikia na tukaruhusu na tukatoa vielelezo vyote hata vya ziada vilivyotakiwa ili waambiwe kuna wizi au hakuna wizi. Nashangaa leo wanaposimama wale wale wanasema kwamba anayetakiwa kuthibitisha siyo CAG, mnakula matapishi yenu leo? Kwa hiyo, lazima tu tuseme ukweli, tuseme wazi ndicho walichokihitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye taarifa ya Kamati ukurasa wa 18, aliyejibu hakuwa PST, hakuwa Paymaster General alikuwa ni Msaidizi wa CAG. Alisema: “... The difference of Tanzania Shillings 1.515.18 resulted from factors such as differences in information reviewed and adjustments passed by management...”. Mimi tarehe 20 mbele ya Bunge lako Tukufu nilisema wazi kwamba haya yamesababishwa na Ofisi ya CAG kutumia budget execution report ambayo haina adjustments. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndicho nilicholiambia Bunge lako Tukufu kwa kuwa nilikuwa naamini wataalam wangu ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango wako makini, hawana tatizo lolote kuhakikisha rasilimali za Taifa hili zinasimamiwa ipasavyo. Naomba niwaambie Watanzania waendelee kumuamini Dkt. John Pombe Magufuli, waendelee kumuamini Dkt. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, waendelee kuwaamini watumishi wote wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Katibu Mkuu Bwana Dotto James. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi sina wasiwasi wa kuaminika mbele ya Watanzania, wananchi wa Jimbo la Kondoa waliniamini. Kwa hiyo, naamini naaminika sina tatizo. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuondoka hapo tunakwenda kwenye hadidu za rejea. Mheshimiwa Catherine, shika hadidu za rejea kwenye taarifa uliyoitumia kutudanyanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye taarifa ya Kamati, twende kwenye aya 2.2.2.2, ukurasa wa 26, nini Kamati imesema, naomba kunukuu: “CAG alifanya hitimisho kuwa utekelezaji wa awali na wa sasa unafanana” Watanzania mnajua nini kilikuwa kinatafutwa kwenye hili? Walikuwa wanatafuta kuthibitisha rumors zao mitaani kwamba kuna pesa zinazotumika bila kufuata kanuni na taratibu na Katiba ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, anawathibitihia hapa CAG na ili tuweze kumuelewa vizuri, CAG page ya 20 kwa wale wenye taarifa yake someni kaandika nini. Tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani, Katiba ya nchi haijavunjwa kwenye matumizi ya fedha za Serikali. Hicho ndicho kinachotafutwa na sasa wamedhihirishiwa wanakuja na hoja zisizo na mantiki yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda kwenye 2.2.2.3, page hiyo hiyo ya 26, nini kilisemwa na conclusion ni nini? Kwa nini tuondoke kwenye hoja? Nilisema asubuhi reallocation between vote siyo kazi ya CAG, ni kazi ya Waziri wa Fedha na Mipango kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini CAG ameandika, ukurasa wa 16, Mheshimiwa Zitto fungua, recommendation, alichokisema: We also recommend that, the Treasury ensure that the Minister’s approval, it is the approval of the Minister not of the CAG, not of the Bunge. Kwa hiyo, haya yote yamekwenda ku-cancel uongo wote mtaani leo tunarudi na 2.4 ambayo haipo popote kwenye taarifa ya CAG, haipo popote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, limeongelewa jambo moja hapa la warrant and exchequer issue notification. Hili kwa kuwa Mheshimiwa Hassunga hakulisema naomba nitoe darasa. Liko hivi, exchequer issue warrant ni nini? Exchequer issue warrant ni nyaraka inayoandaliwa na Mhasibu Mkuu wa Serikali kwenda kwa Governor wa Benki Kuu ya Tanzania baada ya idhini ya Mlipaji Mkuu ili ahamishe fedha kutoka akaunti ya mapato kwenda kwenye akaunti ya matumizi. Inapoingia kwenye akaunti ya matumizi kama yule ambaye aliiandika hii pesa kwenye bajeti yake hajatuletea taarifa inayothibitisha kutumia pesa hii hawezi kupelekewa exchequer issue notification. Mhasibu Mkuu wa Serikali anapoandaa exchequer issue reports hii haiwezi kuingia kwenye ripoti yake kwa sababu haijatumiwa na mtu anayetakiwa kutumia. Kwa hiyo, hili lieleweke wazi, tuwaachie wenye CPA zao waongee kuhusu CPA zao lakini wakiwa na uhakika wa nini kinachotakiwa kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi/Vigelegele)