Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya Uwekezaji, kwa hiyo, mchango wangu utajikita zaidi kwenye eneo hilo la uwekezaji.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba dakika zangu uzitunze. Ni Mjumbe wa Kamati ya Uwekezaji (PIC) na ninapenda mchango wangu uelekee huko kwanza. Kama tunavyofahamu kwamba lengo kubwa la mashirika ya umma haya ni kukuza mtaji ni kukuza ajira, kupunguza umasikini na kukuza uchumi wa Taifa. Tulitegemea kwamba kwamba mashirika haya yale ambayo siyo ya Muungano, mambo haya ya fursa hizi za ajira hupunguza umaskini utaenea kwa Tanzania nzima. Lakini bahati mbaya kwa masikitiko taasisi nyingi za Muungano ambazo tunategemea kueneza ajira hizi Tanzania nzima zimejikita kwenye upande mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natolea mfano, tuna taasisi ya Kituo cha Mikutano ya Kimataifa (AICC) kituo hiki kiliazishwa mwaka 1977 mpaka leo tunavyosema kituo hiki kina umri wa miaka 42, kituo hiki dhamira yake ni utalii wa mikutano ya kimataifa. Rasilimali kubwa za kituo hiki ziko upande mmoja wa Muungano, ajira kwa upande mkubwa unatoka upande mmoja wa Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile fursa au tunasema fursa za tunaweza tukasema huduma za kijamii zinazotolewa na kituo hiki zinatoka upande mmoja wa Muungano. Sasa tulitegemea kwamba kituo hiki kwa sababu shughuli yake kubwa ni mikutano ya kimataifa na kwa sababu kule Zanzibar kuna fursa nyingi, kuna maeneo mazuri, kuna mazingira mazuri ya kuweka uwekezaji, nilitegemea kwamba kituo hiki cha kimataifa kitatoa branch yake kule ili na wale wa upande wa Zanzibar wapate fursa nao za kupata ajira, kupunguza umaskini na kukuza uchumi wa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bahati mbaya tukihoji hapa kwa nini fursa kama hizi hazipelekwi, kwa nini hatutajengewa hili jengo la mikutano angalau ya kimataifa Serikali inasema kwamba mata tunakuja kujenga Dodoma, mara tunajenga Mwanza mara Mtwara sasa tunauliza kujengwa kituo hiki Dodoma kama siyo Zanzibar kitatusaidia kitu gani? Tunaomba sana Serikali huduma hizi za mashirika ya Muungano yapendelee pia kwenda kule Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye Bodi ya Wakurugenzi, nipo katika Kamati kwa muda wa miaka mitatu sasa nikiangalia Bodi za Wakurugenzi kwa kiasi kikubwa bodi zinazokuja katika Kamati hatuoni kwamba inawakilisha Muungano. Wajumbe wote wa Kamati wanakuwa upande mmoja wa Muungano, sasa tulitaka na wale wajumbe kutoka Zanzibar ambao wamo katika bodi ya Muungano wawe pia katika Kamati wanapoitwa na Kamati ya Uwekezaji ili waje washuhudie yale mambo ambayo yanaelezwa na wenzi wao kutoka huku Tanzania Bara, je, ni sahihi au siyo sahihi? Ili na sisi tupate kuwahoji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoka hapa nakwenda kwenye masuala ya TBS (Mamlaka ya Viwango), kazi ya shirika hili ni kukuza uchumi kupitia kulinda usalama wa Tanzania kwa kuhakikisha kwamba wanatumia chakula ambacho kiko salama. Lakini tatizo linalowakabili Shirika hili la TBS ni kwamba lina upungufu wa wafanyakazi, mpaka kufikia mwezi Novemba, 2018 shirika hili lilikuwa na wafanyakazi 456, shirika hili linahitaji wafanyakazi takribani 750 ukiangalia kazi ya shirika hili ukubwa wa eneo la Tanzania mahitaji wanayostahiki kuhudumiwa watanzania ni kwamba kiwango hiki cha wafanyakazi ni kidogo. Vijana tunao wengi wanaomaliza kwa hivyo wapewe fursa za ajira kwenye shughuli ili hili shirika liweze kufanya kazi yake kiufanisi.