Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kutoa mchango wangu kwa siku ya leo.
Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutumbua majipu na kuhakikisha kwamba itapofika Julai aanzishe hiyo Mahakama ya Mafisadi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kweli wanaweza wakasema kulikuwa na mahakama, Mahakama tunazoziona, mimi naishi Dar es salaam, naona kuna Mahakama Kuu, kuna Mahakama ya Rufaa na kuna Mahakama ya Kisutu sijaiona Mahakama ya Mafisadi iliyo wazi, Mheshimiwa Rais ajitahidi kwa kila liwezekanalo alete sheria hapa ya kuanzisha Mahakama ya Mafisadi.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais, kwa kututeulia Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Waziri wetu mahiri, muelewa na anatosha kwa nafasi hiyo. Lakini pia nawapongeza Waheshimiwa Makatibu Wakuu. Waheshimiwa Makatibu Wakuu wamewekwa kulingana na elimu zao na taaluma zao katika Wizara hii na nina imani kabisa kwamba watafanya kazi nzuri sana kwa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wangu hapa duniani kuna matatizo mengi, wewe ni mwalimu, umewafundisha wengi sana lakini kuna baadhi yao watakushukuru na baadhi yao watakubeza. Hayo yote ndiyo mzazi anayopata na ndivyo mzazi alivyo. Unapozaa unaweza ukazaa mtoto mwema na mtoto mbaya yapokee, lakini Mwenyezi Mungu atakulinda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie suala zima linalohusu utumbuaji wa majipu. Katika hotuba ya Upinzani wameeleza kwamba kuna baadhi ya Mawaziri, Wakuu wa Mkoa wanatumbua majipu wakati hawana mamlaka, hiyo siyo kweli!
Mheshimiwa Naibu Spika, utumbuaji majipu utaendelea kufanyika kwa yeyote yule ambaye atakwenda kinyume na maadili ya kazi yake, tena utaendelea utumbuaji huu kwa ngazi za aina mbalimbali. Kama kuna mtu ambaye anaona alitumbuliwa kinyume na taratibu au kinyume na sheria ndiyo maana mahakama zipo, mahakama zimewekwa ili mtu apeleke matatizo yake na hata yule ambaye anaona utumbuaji wake umekwenda kinyume ruhusa kwenda mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nichangie kuhusu fedha za Bunge shilingi bilioni sita. Kwanza nilipongeze Bunge kwa kazi nzuri waliyoifanya, wananchi wetu wanakaa chini, mimi natoka Mkoa wa Dar es Salaam, sasa hivi tumeandikisha watoto wengi sana kuna limbikizo la watoto. Watoto wanasoma wakiwa wamekaa chini hivi leo kuna ubaya gani Bunge kutoa shilingi bilioni sita, kutusaidia Wabunge wote tulioko hapa katika Majimbo yetu tupate madawati.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka wananchi wawaone wenzetu hao wakati wanaomba kura walisema wao ni wazalendo kweli kweli, leo nashangaa uzalendo huu wa kukataa hata kupeleka pesa za madawati katika Majimbo yetu. Jamani hivi tunakokwenda tuko sahihi kweli, kuna mambo ya kubeza, lakini kuna mambo mengine tusifanye masihara kwa sababu wananchi wetu wanapata shida, watoto wetu wanahangaika, wanakaa chini wengine wanakalia vipande vya mawe au matofali. Leo Bunge hili, hivi zile shilingi bilioni sita tulitaka tuzifanyie nini?
Mheshimiwa Naibu Spika, ninalipongeza sana Bunge hili kwa kuamua, uamuzi wake ni wa busara na waendelee kama kuna pesa ambayo inaonekana haina kazi watuletee tunahitaji bado vifaa zaidi katika afya ya mama na mtoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nirudi katika Mkoa wangu. Katika mahakama za Mkoa wa Dar es Salaam kuna Mahakama ya Mbagala, mahakama hii ina hali mbaya sana, Mahakama ya Temeke, Mahakama ya Magomeni, Mahakama ya Mnazi Mmoja na Mahakama ya Buguruni. Mahakama hizi zote zina hali mbaya, zina zaidi ya miaka 50 toka zimejengwa, Dar es Salaam ni Jiji, Dar es Salaam ni kioo cha Tanzania, tunapokuwa na Mahakama za aina hii katikati ya Mji, inakuwa ni tatizo na wala haioneshi kwamba tunakwenda mbele kama Jiji la Dar es Salaam. Ninaiomba Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi waangalie kwenye bajeti zao kuboresha Mahakama ukianzia zile zenye hali mbaya Mahakama za Buguruni, Mbagala, Magomeni na ile Mahakama ya Mnazi Mmoja, ziangaliwe kwa jicho la pekee.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika ngazi ya Wilaya, kuna Mahakama ya Wilaya ya Temeke, Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni na Mahakama ya Wilaya ya Ilala. Hizo ni Mahakama za Wilaya lakini hazina hadhi ya Wilaya, niiombe Serikali iboreshe mazingira yale, kubwa zaidi ni zile selo zilizoko katika mahakama hizo. Mahabusu wanajaa mno katika selo zile vyumba ni vidogo, ninaiomba Serikali iwapanulie hivyo vyumba na kuweka madirisha ambayo, yatakuwa yanawasaidia mahabusu katika kuvuta hewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nizungumzie juu ya sheria inayounda Jiji. Kambi ya Upinzani wamesema wamepata Jiji, ndiyo, mmepata Jiji, je, Jiji lile lina faida gani? Mimi ninaiomba Serikali iangalie upya Sheria ya Jiji. Jiji lile ni Serikali ya tatu halina rasilimali yoyote, pale ni utata mtupu, sehemu ilipo Jiji ni eneo la Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Parking ambazo ndiyo mapato ya Jiji zipo kwenye Halmashauri ya Temeke, Halmashauri ya Ilala, Jiji lile ni mgogoro halina rasilimali ya aina yoyote. Nawashangaa wenzangu niliwatarajia leo hapa walete hilo tuliangalie, wao wanafurahia kupata Meya, Meya huyo ataendeshaje wakati hana rasilimali?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tena niungane na Mbunge mwenzangu Mheshimiwa Kiteto kuzungumzia juu ya Sheria ya Mwanamke, sheria hii iangaliwe kwa mapana zaidi kwa sababu Sheria hii ya Ndoa inawaminya sana watoto wa kike, lakini pia..
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba dakika zangu unitunzie.
Ninaomba Sheria hii ya Ndoa iangaliwe tena upya. Kweli mtoto wa kike kwa dunia hii ya leo, Sheria ya Ndoa inasema mtoto wa kike ataolewa akiwa na umri wa miaka 16, bado ni mtoto mdogo sana, ninaiomba Serikali iiangalie kwa mapana yake Sheria hii na iifanyie marekebisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba fursa hii niitumie kukishukuru Chama changu cha Mapinduzi, hususani Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi, kurudisha majina yenye dhana ya fifty-fifty, kweli Chama cha Mpinduzi ndiyo Chama ambacho kinaendeshwa kwa ukweli na uwazi. Imerudisha majina wanawake wawili na wanaume wawili kazi kwetu. Nakipongeza chama changu, kwa uamuzi wake wa busara ambao wameufanya na vyama vingine navyo viige mfano wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, mbona hawa wana vurugu! Tulieni ninyi!
Naomba nimpongeze kwa dhati ya moyo wangu Mheshimiwa Jenista Mhagama ambaye ni Katibu wa CCM Bunge, amefanya kazi yake kwa ubora, kwa uzuri ameliendesha Bunge hili vizuri sana, anaachia gari hili na wengine tuje tufuate jinsi gani amefanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja asilimia mia moja na kura Wabunge wa CCM....